Monday, August 19, 2013

USIKU ULE WA KWANZA WA FUNGATE (HONEYMOON)......Part 5 (FINAL)!!!

Hello rafiki habari yako!
Naamini umekuwa unafuatilia sana habari hii
Iliyoanzia mbali saaana,pande hizi;
 
.......kwa pamoja wote wakamwambia Usijali,ahsante kama tutahitaji ushahidi wowote ule tutakutaarifu,basi meneja akatoka na kuwaacha na wao wakabaki na kuongea kitumishi na kiutu uzima na baada ya mazungumzo ya kina kiasi,basi wote kwa pamoja wakaamua ku……………………………….ENDELEA SASA!
 
 ....kutafuta suluisho kwa pamoja...Basi jambo la kwanza walilolifanya ni kukaa chini na kujadilina kwa kina nini cha kufanya,maana kama kijana akirejea nyumbani sasa peke yake itazua gumzo mtaani na kanisani,hivyo ni bora huyo kijana asafiri kidogo na kwenda kupumzika kwao mkoani angalau kwa siku kadhaa wakati ufumbuzi unatafutwa.
 
Basi walibembelezana hapo na wakawa imara, na hapo mama mkwe na mke wa yule msimamizi wakatoka nje na kuwaacha Yule mtumishi na msimamizi wake wa ndoa kwa muda fulani ili wazungumze kiume na kumsaidia kupanga nguo na zile zawadi kwa ajili ya kutoka hapo hotelini.
 
Naam yule msimamizi wa ndoa akataka kupata stori kwa ufupi,usiku ule ulikuwaje...Basi yule kijana akaanza kumsimulia kuwa tukiwa kwenye gari tunakuja huku hotelini toka ukumbini,Mke wangu alikuwa na hamu sana ya kushiriki tendo hili la kwanza hivyo alikuwa joto sana,na hata tulipoingia tu hotelini cha kwanza ilikuwa ni mashamu shamu kibao...lakini mimi niliazimia kuanza tendo hili la kwanza kwa kuweka wakfu kwanza kwa maombi....hivyo nilimshauri tufanye maombi,na hata tulipoanza yeye hakuomba wala hata kuwa na mimi sana,bali nikiwa ninaendelea yeye alitoka na kwenda kuoga na kurudi na Taulo tu,na kukaa mbele yangu hali ninaendelea kuomba na mimi nikaona hapa ipo shida,kwa hiyo nikazidi kutakasa na kukemea kila aina ya maroho machafu ndani ya mke wangu,baada kumaliza kuomba,kwa muda kama wa masaa mawili hivi nikaenda na mimi kuoga na niliporudi nikakuta mke wangu amepitiwa na usingizi,huku taulo imemfunuka na hivyo akiwa wazi kabisa.
 
Yule msimamizi akauliza ..yaani umefika honeymoon ndio unaanza kuomba? ulikuwa wapi siku zote? na huyo mke mpaka umepewa toka madhabahuni,yaani umekuja kugundua uchafu na maroho ukiwa nae huku hotelini? na hatukatai kuanza na maombi ukiwa honeymoon maana ni ibaada,lakini ndio wewe umeamua kufanya masaa mawili kweli? Jamani unajua kila jambo lazima lifanyike kwa utaratibu na kwa mpangilio tena kwa wakati wake!.....wakati yule bwanaharsi akijitahidi kujitetea, yule msimamizi akasema hapana utetezi katika hili mpaka hapo ulikuwa umeshamtesa sana kihisia na hivyo sio vizuri.
(Naamini na ninyi wasomaji mmepata fundisho katika hili,huwezi kuwa  kwenye uchumba ama mahusiano yeyote yenye kibali cha Mungu na usijue nini cha kuombea,eti mpaka wakati wa honeymoon...na hata kama wewe ni mtakatifu zaidi ya utakatifu wenyewe,lazima ujifunze kufanya kila jambo kwa wakati wake...ya kiroho yawe hivyo na ya kimwili yawe hivyo)
 
 Eeeh endelea kaka...
Basi nilivyotoka kuoga, nakumwona yuko vile nikaona sasa ndio wakati muafaka wa kuendelea na ibaada,basi nikamshtua taratibu,na kabla sijasema neno,aliponiona namuangalia basi basi akanirukia mwilini na kuanza mashamushamu tena,na kiukweli mimi mengine siyajui na yamkini sikuitikia vile anataka labda,basi akiwa anaendelea hapo tukaangukia kitandani nae akawa juu yangu na vurugu hizo,baada ya muda kidogo nikaona niko tayari,basi nikampindua na bila kuchelewa nikaingia...na hapo kuna namna ambayo alilamika...na kusema Mbona hivyo? na sikujua nini mbaya,basi tuliendelea na mimi nilipomaliza tu basi nikaona kwa leo kwasababu ya vurugu zote na mchana,na muda niliotumia kwenye maombi,basi nikajihisi kuchoka naam nikwambia yatosha kwa leo nami nikalala,nilimuona kama amekasirika kiasi ingawa alijifanya kufurahi na hapo alitoka na kwenda bafuni,nafikiri alienda kuoga mmmh!
 
Basi yule best akashangaa na kuumia mno na kusema umemtesa sana mke wako na hata kama sijui sababu hasa,yamkini na hiyo imechangia sana sana,na hapo akaanza kumpa shule kwa kina na hapa nitakuwa kwa ufupi shule yenyewe;
 ( Wanawake na wanaume wametofautiana sana kimaumbile,kihisia na kimuundo...wakati mwanaume akipata tu wazo au hamu ya kufanya mapenzi basi saa hiyo hiyo ama ndani ya muda mfupi sana huwa tayari lakini wanawake hisia zao hupanda taratibu sana hivyo anahitaji maandalizi ya kutosha,kwanza utayari kisaikolojia kisha juhudi za kuamsha hisia hizo....na wanaume wengi huwa hawajui kuwa wanawake nao hufika katika kilele cha furaha yao (ogarsm), na hivyo wengi hujifikiria wao tu,hivyo wanavyomaliza tu wao basi wanadhani ibaada imekwisha....kuna mamilioni ya wanawake duniani wanabakwa na waume zao kila siku,naam wengine wana miaka mingi kwenye ndoa zao na wana watoto lakini hawajawahi kufurahia tendo la ndoa hata kidogo....Mungu ametoa zawadi ya tendo la ndoa ili kwanza wanadamu walifurahie na matunda yake pia ni kupata watoto. Ndoa nyingi zina ugomvi sana hata wanandoa kutoka nje ya ndoa zao sio tu kwasababu shetani anawaendesha,hapana ila kutoridhishana ndio moja ya vyanzo vikubwa na ukiona unaanza honeymoon kwa majonzi basi huwezi kuifuta hiyo picha maishani mwako na mbaya zaidi ni pale dada ambaye alikuwa mfukunyuku huko duniani na hivyo anajua halafu mume hafiki pale juu,basi kumshika Mungu inakuwa hati hati....hivyo ni vema kumuandaa mkeo,angalau dakika 45 kabla ya tendo ili kujenga mazingira ya kibaiolojia ya utayari wake ili nae afanye bila kuumia na afurahie tendo hilo pia....ukiwa umeoa huna haraka ya kukimbia,maana huyo ni mkeo tu na ndio maana ya honeymoon...it is a sex orientation and affairs foundation....BASI IMEMPASA KILA MTUMISHI KULITAFAKARI JAMBO HILI)
 
Basi endelea kaka,naamini umenielewa(Alisema msimamizi)
Oooh kumbe! basi nitakuwa nimemkosea sana na kumuumiza aisee, Dah Mungu anisamehe sana kwakweli maana sikuyajua yote haya na wala sijawahi kusoma popote kujua siri hzi....Eeeh basi nadhani akawa huko bafuni na mimi nikalala,lakini baada ya muda nilikuja tu kushtuka na kusikia mlango ukigongwa na niliposhtuka nikakuta pajama yangu iko wazi na yeye amelala uchi tena,bila mpangilio (mpaka hapa mtumishi hajui kama mke wake alizimia)...basi nikawasikiliza pale mlangoni na walikuwa ni wahudumu wa hoteli na walidai kuna tatizo chumbani kwangu,lakini mimi niliwaambia hakuna shida na wao wakaondoka,basi namimi nikaenda washroom na niliporudi nikamlaza vizuri,na mara akashtuka na huku anaendelea kama kulia hivi,lakini kwa kuwa nilikuwa nimechoka sana nikajipumzisha na kuadhimia kuongea nae asubuhi,basi nikalala na ndio mpaka niliposhtuka asubuhi na kuona pajama yangu imefunguliwa tena na mke wangu hayupo na niliamshwa na simu na ndio ninyi mkaja...ila pia nilidhani labda mke wangu hapendi nywele nyingi ambazo nimefuga kichwani pamoja na huku, na kwangu mimi zilikuwa hazina shida maana zinapata matunzo lakini kwasababu ya mke wangu niliadhimia kuzinyoa pia.
 
Basi yule best akamuuliza unafugaje nywele nyingi hivyo sehemu za siri? au ndio unadhiri? anyway mpaka hapo ninapata picha ingawa bado sijui hasa nini tatizo maana mke wako hajasema kitu,jipe moyo tu kaka,naamini haya mambo yatapata ufumbuzi tu na yatafika mwisho.
 
Naam wakamalizia kupanga mizigo,nayo wakaitoa nje,wakafanya malipo na kuwaombea msamaha wale wafanyakazi na mlinzi,kama uongozi wa hoteli uliwasamehe au laa sijui,ila mimi ninachojua ni kuwa hatimaye zawadi alienda nazo mama mkwe kwa mujibu wa makubaliano na huyu kijana akaenda zake kwao Huko mkoani(naomba nisitaje mkoa) na habari za chini chini zikavuma lakini sio kivile na baada kama ya wiki mbili yule mtumishi akarudi na akawa haonekani saaana na yeye ndiye alisoma ule ujumbe wa mke wake na hakumwambia mtu maana alijua siri nzito. alijitahidi kuwakwepa watu na hata waliomfikia alijitahidi kuuma maneno na siku zikasonga kwa neema za Mungu. Baada ya miezi mitatu yule dada alirudi kwao na mama yake alifurahi mpaka akatoa machozi,hakuweza kumfokea zaidi ya kuonyesha kutokufurahia kabisa jambo hilo maana limemtia aibu mama yake,na hapo baada ya kubanwa sana akaamua kusema mkasa mzima na ni kwanini alikimbia........ITAENDELEA!!!
 
(Hapa ni muhimu kukazia sana kwamba ndoa ni makubaliano ya hiari ya watu wawili na sio msukumo wa watu wa nje kama wazazi na marafiki,kama umempenda mtu na ukaamua kwa dhati kuoana nae basi uutumie muda wa uchumba vizuri kufahamiana,sijasema kujuana kimapenzi hapana! ila kuna mengi mnaweza mkajadili na hata ukajua mtazamo,uelewa na uzoefu wa mambo mengi ya kijamii na hivyo kujua namna ya kuendana nae...na kama ukikaa vizuri na Mungu,lazima akujulishe mambo yote yaliyo sirini sawasawa na kutaka kwako kujua sawasawa na imani yako kwa Mungu na kwa kadri ya imani na nguvu ya Mungu itendayo kazi ndani yako,sop muda wa uchumba mnawaza outing,beach,movie na mnashindwa kuyatazama maisha katika upana wake....NAJUA KUNA MTU HAPA ANATAMANI KUNIRARUA,HAYA NGOJA NISIWAKWAZA HADITHI INAISHA NAMNA HII......)
 
.....MALIZIA!!!  
 Kwanza akaomba msamaha sana kwa mama yake na kwa wote kupitia mama yake na taratibu akaeleza ya moyoni mwake.....Mama ni kweli nampenda sana "X" na nilikubali kuolewa nae kwa moyo mmoja,lakini yeye anafanya kila jambo lionekane ni la kiroho na kwasababu ya ushamba mambo mengi sana hajui na ameishia kuniumiza tu siku ile ya kwanza...mmmh! (Mama akakaa kwa makini na kutega sikio,eeeh sema mwanangu)
.....Baada ya yote hayo niliyosema wala haikunisumbua sana ila wakati tunafanya,bila hata kuniandaa aliniingilia,na ukweli nilisikia maumivu sana kwa jinsi ilivyokuwa kubwa na baada ya muda mfupi alimaliza na kulala,lakini kilichonishangaza mbona hata alivyomaliza yeye,ingawa hakujali kama mimi nimefika au laa,mbona sikuona badiliko ya hiyo .....yake,basi baadae niliamua nimchungulie nijue hasa kwa undani,basi alipolala nikamfungua na kumchungulia na dah! hapo nikashutuka kuona hiyo nanii kubwa na bado imesimama na rangi yake haifanani ya mwili wake,basi hapo nilizimia na baadae nilizinduka na kuanza kulia,na kwasababu sikuamini nilichokiona,nikasema nitathibitisha tena,basi mara hii alipokuwa amelala nilifunua tena na kupapasa mkono,lakini mara hii cha kushangaza ni kuwa, ile kitu haikuwepo na hapo nilipogusa nikaona tu kakitu kadogo sana ndani ya minywele na hapo nikahisi kama naona mazingaombwe,na baadae niliona maisha haya siwezi kuishi mpaka kufa ndio nikaamua kuondoka!
 
(Najua unatamani kujua nini hasa kilikuwa pale ndani....ndio ukweli ni kuwa mtumishi yule alikuwa ana maumbile madogo sana (kidole chanda) na hivyo kwa ushauri wa marafiki wa karibu aliamua kununua Dido (artificial P.) na kuamua kuuvaa pale anapofanya bila kumwambia mkewe ukweli,na hiyo ndio iliyomgarimu sana kijana huyo....ni muhimu sana kuomba ushauri wa karibu sana kwa watu unaowaamini ikiwa mwilini mwako kuna upungufu au ulemavu,isije kuwa na wewe unajua kabisa huwezi kuzaa kisha unaoa au kuolewa na kuanza kumsumbua mwenzako kwa maombi na tabu hali unajua wapi ulijikwaa....kwa habari ya maumbile,yawe makubwa au madogo,ninaamini kuna namna unaweza kusaidiwa na madaktari na washauri kabla ya kamua kuoa au kuolewa)
 
N.B; Ninaomba mnisamehe kwa lugha ya kuumiza hisia zenu ila naamini kuna mtu kasaidika katika hadithi hii,hatuwezi kuandika kila kitu hapa ila Mungu akupe hekima ya kujifunza kila ambacho ingefaa ujifunze.
 
....KAMA YULE KIJANA ALIOA TENA AMA KUONANA NA MKE WA KE TENA MIMI SINA HAKIKA,ILA NINAJUA JAMBO MOJA TU KUWA MPAKA SASA WATU HAWA HAWAKO PAMOJA!
 
SAWASAWA NA Wafilipi 4:8...."Hatimaye ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa njema, ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote,yatafakarini hayo."
 
 MUHIMU SANA TOKA KWA MWANDISHI;
1.Sijaandika habari hii ili kukushawishi wewe kufanya sasa, ila nataka upate mwanga mkubwa zaidi kuwa mambo ya ndoa ni makubwa zaidi ya vile unavyowaza,hivyo kama unaomba Mume au Mke basi hakikisha unamwamini Mungu kwa 100%
2. Ni marufuku kujaribu kufanya,kuonyeshana hata kushika sehemu za siri za mwenzako kabla ya ndoa
3.Sitaki utumie akili yako kuikabili hofu ambayo imejengeka ndani yako baada ya habari hii ,ila nataka umwamini Mungu kuwa ukiwa mwaminifu na msikikivu Bwana atakufunulia yale yote ya sirini hata ambayo mwenza wako amekuficha.
4. Hakuna raha yoyote honeymoon kama ulishaanza kufanya mapenzi na mwenza wako huyo kabla ya ndoa, na hata wale wanaoenda honeymoon, sio lazima muanze kufanya siku hiyo hiyo mnayofika...kwa kuwa mnakuwa mmechoka na hamjuani vema hapo kitandani,basi mnashauriwa kupumzika na pale mnapoamka na kuwa na nguvu fresh,baada ya kuoga asubuhi, ndi hapo sasa mnaweza mkaanza ibaada kwa michezo na mashamushamu ya ha hapa na pale...hapo mtakuwa mnaandaa hisia zenu na kupata nafasi ya kujuana kila mmoja anafurahia zaidi nini,wapi na kwa vipi?
5. Ni marufuku kutumia hayo mapicha ya ngono kama mwalimu ndani ya ndoa,hizo picha zimechezwa kibiahsra na nyingine ni kazi ya kumpyuta,humo ndani watu hutumia madawa,na hufanya mengi kwa influence ya kipepo,sasa usije ukaaingiza tabia za kikahaba na maroho yake ndani ya ndoa yako
KUNA NAMNA YA KUFANYA NA KUFURAHIA TENDO LA NDOA NDANI YA NDOA KWA AJILI YA KILA MTU, BILA KUJALI MAUMBILE,VIMO WALA CHOCHOTE, MUHIMU NI KUKUBALI KUFUNDISHIKA NA KUWA TAYARI,VIPO VITABU VIMEANDIKWA NA WATUMISHI WA MUNGU...UKIFIKA WAKATI WAKO BASI NENDA KATAFUTE KWA BOOKSHOP,MFANO "TENDO LA NDOA" NA VINGINEVYO!!!
 
*********MWISHO (THE END)************* 

Kwa Maoni, Ushauri na Neno lolote,hata kama ni Stori ya kweli toka Mtaani kwako au Maishani mwako basi check me out!!!
+255 713 883797
@Imedhaminiwa na http://quality-love.blogspot.com
(c)2013
  

Monday, August 12, 2013

TESTIMONY TO LEARN FROM.......UNEMPLOYED CHRISTIAN CHUKWUDI MARRIED AGAINST FRIENDS' ADVICE!!

A Guy who has no job got married to a banker, despite his fears and several advices that it’s not good to marry without a job. Every month the girl would give the guy her full salary of N135k after removing her tithe.

The guy would give the wife N20k for personal upkeep and the guy determined what happened to the remaining money. This happened for three good years. There was happiness in the family and the wife never refused to do her primary home duties for that 3 years, despite wrong advice from friends that ‘you can’t be paying the bills and still be doing all the work’.

There was a particular month the guy used about N70,000 to travel from state to state for different interviews.He finally got a job witha good firm in Port-Harcourt. His salary was N600,000 monthly for a start. He bought his first car (a brand new) for N4.5m, he gave d wife the car key, and continued to take public transport to work for about two years. Then he bought the second car for N6 million. Then he took the keys of the first car and gave his wife the keys of the second car. They were very happy. They eventually moved into their own house after few years.One day, the wife was looking for some documents. Then she stumbled on a file neatly hidden, when she opened it, she saw her wedding picture when she was very slim in the first pageof the file.

She then saw that the document to the purchase of the land and every other thing in the house were all written in her name! At the last page was the husband’s wedding picture and a note written by him: ”MY WIFE IS ALL I HAVE GOT. NOT EVEN THIS HOUSE WORTH N24M AT THE TIME I BUILT IT IS MINE”.

Tears started to roll down her eyes as tried to put the documents neatly as she saw them and walked back to the kitchen. This couple got married in 1998. Last Sunday was their wedding anniversary with three children, two boys and a girl. True LOVE still exists till this day. Are you sure the love you have for your partner can be compared to this one you just read? No matter what, remember you chose each other. So share. It doesn’t matter who puts food on the table.


SOURCE; http://www.nairaland.com/1161751/unemployed-christian-chukwudi-got-married

USIKU ULE WA KWANZA WA FUNGATE (HONEYMOON).........Part 4!!!



Hello rafiki habari yako!
Naamini umekuwa unafuatilia sana habari hii
Iliyoanzia hapa



SAWASAWA NA Wafilipi 4:8...."Hatimaye ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa njema, ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote,yatafakarini hayo."

NDIO NA MIMI NAWALETEA SIMULIZI HII ILI MWISHONI KWA PAMOJA TUTAFAKARI;

ILIPOISHIA PART 3;
....mara alivyofunua tu hivi na kumwacha mumewe Uchi kabisa....Binti alishtuka kwa mshangao na kusema "Mamaaaa" na hapo akaangukia kitandani na kuzimia...............

ENDELEA SASA NA PART 4; 
Na kwasababu mume wake alikuwa amepitiwa na usingizi wa kuchoka,hata uliposikika ule mshindo pamoja ile sauti ya “mamaaa”, mume wake hakusikia ila inahisika kuwa kuna watu walisikia chumba kingine na hivyo wakaamua kugiga simu mapokezi na kuwatarifu wahudumu wa Hotel, na hiyo iliwalazimu wahudumu wa Hotel kugonga vyumba kadhaa ili kujua hasa ni wapi ilikuwepo shida….na walipogonga chumba No 307, basi toka usingizini Yule mtumishi akashtuka kwa nguvu na kuona mke wake amelala uchi kabisa tena sio kulala kivile ni kama amejibwaga tu,basi akamfunika haraka na kwenda kusikia anayegonga mlango……na alipofungua akashangaa kuulizwa kuna shida gani humu mbona kuna sauti ya mshtuko imesikika huku? Basi haraka akajibu mke wangu huwa anashtuka shtuka hata akiona mende tu, sasa yamkini kuna jambo limeshtua,ila hakuna tatizo lolote lile na kama ikiwepo shida nitawapigia simu,samahani sana kwa usumbufu….basi wale wahudumu wa hotel  wakaondoka lakini kwa shingo upande, naye akafunga mlango na kurudi ndani.

Aliporejea akawa na maswali mengi sana kichwani maana hata hakujua nini kimetokea na basi alichokifanya ni kumbeba mke wake na kumlaza vizuri kitandani….na akamlaza akiwa anatazama juu,basi kabla hajamfunika alibaki kwa sekunde kadhaa akiwa anamshangaa Mungu kwa uumbaji wa mke wake….na baada ya muda akawa ameshikwa na haja ndogo basi akakimbia mara moja chooni, na alipofika huko kwanza akashtuka sana kuwa ile pajama yake ilikuwa wazi, I mean ilikuwa imefungunguliwa na hapo akapata kigugumizi cha kuwaza…ina maana na wale wahudumu wawili wa hoteli walimuona utupu wake? Lakini hakufungua mlango wote wa chumbani mmmh yamkini hawajaona kitu….na alipotaka kukojoa akagundua kuna upungufu Fulani anao,basi akamaliza haraka na kunawa mikono na kurudi haraka na kuanza kuangalia huku na kule na kumbe ilikuwa chini ya kitanda na ilianguka pale alipostuka kwa nguvu wakati mlango wa chumba cha hoteli kikigongwa na hapo akaokota na kuweka kwenye droo ya kitanda chake, na hapo akawaza zaidi ina maana mke wangu ameona?

Basi akiwa na mikono mibichi akawa amemshika usoni kwa namna ya kumfuta machozi na kupitisha mikono mwilini mwake kwa namna ya kubembeleza na muda wote huo asijue ya kuwa mke wake amezimia na hapo akidhani mke wake amelala…..kwasababu ya ubaridi wa mikono ile na Uwezo wa Mungu tu Yule binti akashtuka na kuanza kulia….Jamani hivyo ndio nini? Maana yake nini sasa? Sitaki….sitaki……sitaki…… na kuendelea kulia kwa huzuni, basi huyu mtumishi akashangaa na kuendelea kumbembeleza jamani basi yanazungumzika…..kwa akili ya kawaida Yule mtumishi alidhani mke wake analalamikia Afro ambayo alikuwa nayo kichwani pamoja na ikulu,tena zote zilikuwa zimesheheni na zilikuwa zimetunzwa vizuri….kwa haraka unaweza ukasema labda ni nadhiri ya Bwana ya utumishi kama ya Samson, kwamba asinyoe mpaka hapo kusudi la Bwana litakalotimilika.

Yule dada akanyamaza bila kuongea zaidi nae akawa amekaa pale kitandani kwa kuwaza san asana na mume wake alikuwa ameshalala zamani sana,yaani ule usingizi wa pono, basi Yule dada akaamka na kukaa kitandani asijue afanye nini….Je aombe? Je awaambie wasimamizi wa ndoa? Au amtaarifu mama yake?....Basi akajiambia moyoni ngoja nione tena ili athibitishe kuwa alikuwa anaota au laah!
Basi taratibu akaifungua tena ile kamba ya pajama ya mume wake na kufunua taratibu, na saa alichokiona ni tofauti….”Mmmmmh!” aliguna kwa mshtuko na hapo akapata ujasiri akaingiza mkono na kupapasa,na hapo alibaki ameduwaa na hapo akawa na maswali mengi zaidi ya majibu…..mbona alichokiona hapo kwanza hakifanani na hiki,au hii ndio miujiza ya mtumishi wa Bwana,oooh hapana hakuweza kuvumilia,akamfunika bila kufunga vile kamba ilivyokuwa,akaamka na kuoga haraka na kuvaa jinsi yake na tisheti na kuchukua simu yake,pochi na vile vitu vyake vya muhimu tu na kuacha vingine vyote hapo ndani kama vile shela ya harusi na zawadi zote alizokuwa ameletewa…..na hapo akaandika ujumbe kwa mume wake na kuacha mezani na kuandika ujumbe wa simu kwa mama na wasimamizi wa harusi na kisha akaitoa ile kadi ya simu na kuitumbukiza chooni,ili asiwepo mtu wa kumtafuta…na hapo akabeba kijibegi chake, na kufungua mlango taratibu na kufanya manuva pale mapokezi na getini kwa mlinzi na kuishia zake na hiyo ilikuwa mida ya saa kumi na moja na robo.


Huku nyuma mida ya saa kumi na mbili hivi huyu jamaa alishtuliwa simu zikiita mfululizo na alipoamka cha kwanza ni kuona mke hayupo na hivyo akaenda kuangalia chooni na bafuni, holaa…chini ya kitanda holaaa…basi katika hali ya kuchanganyikiwa akatoka na pajama mpaka mapokezi na wao wakasema hawajamuona mke wake hapo,ila kuna mkaka mmoja tu ametoka alikuwa anawahi safari yake, wasijue ya kuwa binti Yule alifungua mlango mmoja ulikuwa wazi wa chumba alichokuwapo kaka mmoja akiwa hoi amelala kama amekufa na kuchukua ufunguo wa hapo na kuwasilisha mapokezi na hawa wa mapokezi sababu ya usingizi na wao walisema uweke tu hapo mezani…….hivyo Yule mtumishi akachoka na kurudi chumbani kwake haraka,akiwaacha wahudumu wa hoteli pamoja na mlinzi wakizozana na meneja maana wamekuwa wazembe…..

Yule mtumishi aliporejea chumbani akaona simu yake ina miito mikoso (missed calls) zaidi ya hamsini toka kwa mama wa binti,wasimamizi wa harusi,wazazi wake pamoja na marafiki zake wa karibu waliotaka kujua kulikoni maana wengine waliifahamu siri, basi akiwa hajakaa sawa akaona kijikaratasi mezani na anapokifuata ili ajue kimeandikwa nini,mara mlango ukafunguliwa haraka na hapo wakaingia wasimamizi wa harusi yao pamoja na mzazi wa binti akifuata nyuma na hivyo akakichukua kile kikaratasi na kuficha katika mfuko wa pajama na kukaa kitandani kwa kuhamaki,asijue awajibu nini watu hawa wenye maswali mengi yaliyojaa hofu ambayo hata yeye mwenye we hana majibu yake……Basi wakiwa wanatmbea huku na huku na kuuliza swali hili na lile, mama mkwe alibaki tu akilia pembeni kwa huzuni.

Huku chini nako mzozo ulizidi na wale wahudumu wa hoteli wa zamu pamoja na mlinzi kazi ikaota manyasi, na hapo meneja akaja chumbani na kuanza kuomba radhi kwa yote yaliyotokea,alifanya hivyo kulinda hadhi ya hoteli yao na kulinda kibarua chake,lakini mle chumbani kila mmoja alikuwa na lake na sijui hata kama walikuwa wanamuelewa….basi kwa pamoja wote wakamwambia Usijali,ahsante kama tutahitaji ushahidi wowote ule tutakutaarifu,basi meneja akatoka na kuwaacha na wao wakabaki na kuongea kitumishi na kiutu uzima na baada ya mazungumzo ya kina kiasi,basi wote kwa pamoja wakaamua ku……………………………….ITAENDELEA!!!


(Usijaribu kutabiri watu hawa waliamua nini,maana hutajua mpaka nimekujuza. Naam…..Unataka kujua Binti huyo alienda wapi? Alionekana baada ya muda gani? Na alifanya nini aliporudi? Je unajua aliona nini na yeye kudhani ni mazingaombwe? Je nini hasa ukweli wa kile alichokiona na kuamua kuikimbia ndoa yake? Je kijana alifanya nini baada ya hapo? Kanisani alionekanaje? Kwa haya pamoja na USHAURI WA MWANDISHI sawasawa na Maandiko basi….Usikose sehemu ya 5 na ya mwisho ya hadithi hii yenye ukweli na mafunzo ndani yake, kwako wewe ambaye hujakutwa na dhahama ya namna hii, Ahsante kwa kufuatilia USIKU WA KWANZA WA FUNGATE!!

INALETWA KWENU NA;
KING CHAVALA-MC
+255 713 883 797
(c)2013

Tuesday, August 6, 2013

WATOTO YATIMA WA HOCET WANA UHITAJI WA CHAKULA MKUBWA SANA...SHOW LOVE PLEASE!!!!

SHALOM!
HABARI ZENU WAPENDWA!!
NINAAMINI MNA MOYO WA UPENDO, TENA WA KUWAJALI WENGINE KULIKO NINYI, NA HATA ZAIDI BIBLIA INASEMA UPENDO WA KWELI NI ULE WA KUWAPENDA WENGINE ZAIDI.
*****HANANASIFU ORPHANAGE CENTRE (HOCET)....HAWANA CHAKULA KABISAAAAA NA WEWE NA MIMI PEKEE NDIO TUNAWEZA KUWALISHA KWA SIKU 120, KABLA HAWAJAANZA KUJITEGEMEA****
LEO NINALO OMBI MAALUM KWENU, NI MUHIMU SANA SANA....KUNA KITUO KIMOJA CHA KULELEA WATOTO YATIMA (WATOTO WA MUNGU), KITUO KINACHOENDESHWA NA WATU TU WALIOJITOLEA, NA HAPO AWALI KILIKUWAQ KINAFADHILIWA NA WAZUNGU FULANI, LAKINI BAADA YA KUONA WATOTO HAO WAMEKAZANA NA MUNGU NA HAO WAZUNGU (WAFADHILI) WAKAWEKA MASHARTI, ETI KAMA WAKITAKA WAENDELEE KUPOKEA MISAADA YAO BASI WAACHANE NA HAYO MAMBO YA YESU YESU....NA KWA KUWA HAKUNA BABA MWINGINE ZAIDI YA MBINGUNI NA HAKUNA  NAMNA BINADAMU ANAWEZA KUISHI KWA MISAADA YA BINADAMU MWINGINE BAADA YA KUMKANA MUNGU WA KWELI.
 
SASA WATOTO HAO WAKO KWENYE ENEO LAO LA SHULE WANASOMA NA WANAYO MIRADI AMBAYO BADO HAIJAANZA KULETA FAIDA ILI WAWEZE KUJIENDESHA WENYEWE, NAHIYO ITAKUWA HIVYO TU BAADA YA MIEZI MITATU AU MINNE KUANZAIA SASA.
WATOTO HAWA KWA SASA HAWANA CHAKULA KABISA, NA HATA LEO WAMEKULA KWA MSAADA WA KIJANA MMOJA ALIJITOLEA YEYE BINAFSI NA FAMILIA YAKE....MBALI NA GHARAMA NYINGINE ZA UENDESHAJI KAMA MISHAHARA/POSHO ZA WALIMU;
************************************************************************************************
KITUO HIKI KINATUMIA UNGA KILO 30, MAHARAGE KILO 14 NA SUKARI KILO 5....NA IKIWA NI WALI,BASI HUHITAJIKA KILO 30 ZA MCHELE KWA MLO MMOJA....NA PIA UNAWEZA KUCHANGIA MAFUTA NA FEDHA KWA AJILI YA VITU VINGINE VINAVYOWEZA KUHITAJIKA.
************************************************************************************************

NINAAMINI KWA MSAADA WA WATANZANIA WOTE WENYE MAPENZI MEMA NA WATOTO WA KITANZANIA, WATOTO HAWA HAWATAKOSA CHAKULA KWA SIKU HIZI 120 ZA MPITO KABLA HAWAJAANZA KUJITEGEMEA WENYEWE, SIO LAZIMA ULETE MSAADA MKUBWA SANA, LAKINI NAAMINI UNAWEZA UKAJITOLEA CHAKULA KIASI JAPO KWA SIKU MOJA TU KAMA SIO TATU, YAWEZA KUWA WEWE BINAFSI AU KAMPUNI AU FAMILIA AU KANISA, LAKINI NINACHOKIAMINI NI KUWA KAMA KWELI TUNAAMINISHA KUMPENDA MUNGU NA KUWAPENDA WATOTO WATANZANIA TENA WANAOLELEWA KATIKA MALEZI YA KIMUNGU BASI LAZIMA WATOTO HAWA WATAISHI BILA HOFU YA CHAKULA KWA SIMU HIZI 120, NA KWA HAKIKA BWANA ATAKUBARIKI SAWASAWA NA IMANI YAKO KWAKE
YAK 1:27 "....DINI ILIYO SAFI ISIYO NA TAKA MBELE ZA MUNGUBABA NI HII, KUWATAZAMA WAJANE NA YATIMA KATIKA DHIKI YAO NA KUJILINDA NA DUNIA PASIPO NA MAWAA"
 
MSAADA HUO UNAHITAJIKA SANA SANA, NAAM KWA NAMNA YOYOTE ILE UNAYOWEZA KUCHANGIA BASI USISITE,FANYA HIVYO...SADAKA YAKO YA KUWALISHA WATOTO HAWA HAITASAHAULIKA HATA KIDOGO, UNAWEZA KULETA MCHANGO WAKO WA CHAKULA PALE OFISI ZA NIIM COMPUTERS, MOROCO HOTEL AU UKATUMA MCHANGO WAKO WA FEDHA KWA NJIA YA SIMU, NAAM KWA MAULIZO ZAIDI 
TAFADHALI WASILIANA NA WASIMAMIZI NA WARATIBU WA ZOEZI HILI KWA NO.
0713 26 1425 na 0754 527955, pia 0783 757051
KWA NIABA YA WASIMAMIZI WA KITUO HIKI NINAWASHUKURU HATA KABLA HAMJAFANYA JAMBO LOLOTE MAANA NAAMINI UMEGUSWA NA UKO TAYARI SASA KUWASAIDIA WATOTO HAWA...KAMA TUNAWEZA KUCHANGIA SHEREHE ZA HARUSI, NAFIKIRI HATMA YA WATOTO HAWA NI ZAIDI,MUNGU AKUBARIKI UNAPOMSHIRIKISHA NA MWENZAKO!!
 
Imeandikwa na
KING CHAVALA MC
KWA UDHAMINI MKUBWA WA CHAVALA IDEAS PLATFORM.

Monday, August 5, 2013

USIKU ULE WA KWANZA WA FUNGATE (HONEYMOON)- Part 3

Habari zenu ndugu wasomaji na wafuatiliaji wa Mkasa huu uliotokea mkoani Pwani,pale kibaha ambapo binti mmoja alimtoroka mume wake baada ya usiku mmoja tu wa honeymoon.

Tuliazia hapa...http://quality-love.blogspot.com/2013/06/usiku-ule-wa-kwanza-wa-fungatehoneymoon.html
 
habari zenu naamini mko wazima sana, na naamini bado unafuatilia habari hii ya binti huyu aliyetoroka usiku ule wa kwanza wa fungate....habari iwe chachu kwako kujifunza na kuzingatia mambo yale ambayo yamkini huyajui lakini yamewagharimu wenzako wengi na hata sasa ndoa zao zina shida....KARIBU SANA!!
 
ILIVYOISHIA Part 2. 
http://quality-love.blogspot.com/2013/07/usiku-ule-wa-kwanza-wa-fungate.html

.....na huku baada ya maombi ya mtumishi ya takribani masaa mawili, nae akaenda kuoga na kurudi akiwa na pajama na kumkuta mkewe amepitiwa na usingizi akiwa amelalia mgongo akiwa na Taulo tu, basi hivyohivyo Mtumishi huyo akaamua kum...........INAENDELEA HAPA CHINI!

NAJUA KILA MMOJA ALIKUWA NA HISIA NA MTAZAMO WAKE JUU YA WATU HAWA, BAADA YA KUJUA KWA SEHEMU KILE KILICHOTOKEA USIKU ULE...HAMNA UBAYA YALE YALIKUWA YAKO...ILA UKWELI MWENYEWE NI HUU.....ENDELEA!!

.....shtua kwa kumtikisa kidogo, huku akimwangalia kwa macho ambayo hata yeye mwenyewe alishindwa kuyaelezea; sijui ni macho ya huruma au kuombwa kuonewa huruma,sijui ni wivu au hasira au ndio macho ya mtumishi ya kuomba msamaha...basi yule mke alivyostuka kwa nguvu toka usingizini, akajigeuza kwa haraka na taulo lake likafunguka,hivyo akabaki kama alivyozaliwa....basi huyu kijana alibaki ameduwaa kana kwamba hajui kinachoendelea....akiwa mdomo wazi kwa takribani dakika moja na nusu hivi basi yule mrembo akawa macho kabisa na akawa nae anamshangaa mbona mume wake anamshangaa kana kwamba haamini ni yeye.

    Lazima ikumbukwe kuwa kijana huyu hajawahi kabisa kujihusisha na mambo ya mapenzi zaidi ya zamani zile za utoto wakati akidimba (Hii inadhihirishwa na matendo yake ya wazi kabisa ambayo hayategemewi kutokea Honeymoon)...lakini binti ana utalaamu wa kina kupita maelezo ya kawaida,maana ameshawahi kuruka ruka huko na kisha akarejea kundini, namaanisha akarudi wokovuni na ndio hapo akapata bahati ya kuolewa.

    Basi yule binti alipoona mume wake anamshangaa akaamka na kumvuta mkono kwa nguvu,hivyo yule jamaa akaangukia kifuani kwa mke wake, na hapo mke akamkaba shingo na kumparamia kana kwamba anapanda mti lakini mti ulioinama na hapo binti akawa anajaribu sarakasi zake za mahaba...lakini kijana hakuonekana na ushirikiano saaana japo alikuwa anaweza kujigeuza na kurudia maneno yale yale zaidi ya mara ishirini...."Unajua nakupenda sana Mke wangu"...basi kwa kuwa binti alikuwa na hasira hapo kwanza, nazo zikaisha zote...na mara baada ya binti kumuelekeza mumewe kuwa naomba nishike hapa na hapa, japo kwa woga na mshangao mtumishi akafanya hivyo...japo alibahatisha tu, inaonekana ile injini ya yule mwanamke ilikuwa "ON" na ilikuwa mtelemkoni, yaani alikuwa anasubiriwa mtu tu atoe kigogo uone linavyowaka.

(Samahani kwa lugha hii ngumu, na kama itakuwa kwazo kwa yeyote tusameheane ingawa naamini kila anayesoma hapa  ni mtu mzima na anaweza kuwa anaelewa....kimsingi ashiki ya kufanya mapenzi huanzia kichwani, kama kuna ule utayari na hamu basi ashiki hiyo hupandisha joto la hisia kwa haraka sana...na wakati wa tendo, wanaume hufika mwisho wa hatua moja na kuridhika ndani hata ya dk moja mpaka tano tu, lakini kwa wanawake inaweza kuwa mara tano zaidi ya wanaume...kwa hiyo kuna maandalizi yanapaswa kufanyika ili angalau safari ianzie mahali ambapo wote wawili hawatachelewa kufika. Na kama hawa wawili wakifika kwa pamoja basi jambo hili huwa ni jema sana kwa wote)

    Basi mara tu ya yule jamaa kukumbuka kuwa yeye ni mume wa mtu na kuna kitu anapaswa kufanya, alijigeuza haraka na sasa mwanamke akawa chini na yeye akawa juu...bila kujali mwanamke anaendelea na juhudi gani, na yeye akafungua kamba ya pajama yake na kutafuta mkao wa magoti vizuri, bila kusema neno lolote, kwa pupa na kwa haraka mtumishi  "AkaINGIA"....Na basi kwa sauti ya kulalamika yule dada akashtuka na akalia kiana akisema (Akataja jina) mbona hivyo jamani?...ni dhahiri kuwa alikuwa mtulivu kwa zaidi ya miaka miwili na saa hiyo ukavu ulikuwa upo wa kutosha na ndio maana alilalamika mmh...

     Ndoa ni uvumilivu, basi yule binti akajiachilia na kuchukulia ize na akaona sio sawa kumlalamikia mtumishi wa bwana, maana kwanza hana hakika kama anajua au laah! Basi yule mdada akiwa amemwachia mumewe aendelee na ibaada, huku akawa anafanya juhudi binafsi ili angalau akaribie, basi yule kijana alijisukuma kama mara kadhaa tu,haisemekani wala kuaminika kuwa ilipitiliza mara kumi, kijana akawa ameshamaliza ibaada na kutoa matoleo na kuganda kimya kwa muda kama zile zile video za You-tube zinavyogandaga kwa internet yenye kasi ya chini....hapo kijana alikuwa amekakamaa kama vile kuna kitu kinachofolewa mwilini mwake, lakini kama ujuavyo uzoefu mpya lazima mtumishi atokwe na jasho.

     Jambo la kushangaza, baada ya yeye kutoa matoleo, akafikiri na mkewe na ibaada ishaisha kumbe masikini ya mkewe iko taratibu na ndio kwanza ilikuwa inaanza kuchanganya, ikavurugwa na wakati inataka kurudi kwenye mwendo ule wa kawaida kurudi rahani, basi yule mtumishi Akachomoka na kujifuta kidogo na Taulo na kumfuta mkewe na kisha akafunga pajama yake na kulala kando ya mkewe...yule binti alibaki kushangaa tu....hasira za uchungu zikaanza kuja na hapo mrembo yuko ile heat ya juu kabisa, basi akamwambia mumewe azime taa ili angalau ajisaidie na kusogeza mbele ibaada japo mpaka wakati wa matoleo...mume akagoma akasema hapana tuiache tu....basi yule msicha akaamua kwenda bafuni na huko akajifungia na kuamua kujisogeza manualy mpaka akafika, japo ni dhambi na sio nzuri kihivyo, lakini anasema alifika.

    Alipomaliza akakaa sana huko bafuni na kulia sana, akijaribu kufikiri hivi kweli mume wangu ndio huyu na hii ni siku ya kwanza tu yuko hivi...maisha kweli yataenda....basi mawazo mengi yakawa yanazunguka kichwani....anakumbuka nasaha wakati wa kitchen party...anakumbuka mahosia ya baba na mama...tena anakumbuka ndugu na jamaa waliowahi kuvunjs ndoa...anajaribu kukumbuka mapenzi aliyowahi kufanya huko duniani na akichanganya na wale waliowahi kumtenda....basi anataka kufanya maamuzi magumu...lakini tena anakumbuka mahubiri na mafundisho ya ndoa aliyopitia....ndio ni mpaka kifo kitakapowatenganisha.

   Basi baada ya muda akawa amepata nguvu na ujasiri na akaadhimia na yeye kwenda kumshurutisha tena mumewe ili warudie tena na hiyo ilikuwa mida ya saa tisa usiku...Basi akatoka bafuni akiwa na taulo lake na hapo akamkuta muwewe amelalia mgongo na usingizi umeshamchukua...nae akajiambia nafsini mwake nitafungua pajama hii na kufanya kila juhudi na akiamka tu nakaa juu (Ikumbukwe kuwa  mpaka hapo Msichana huyu alikuwa hajaona sehemuza siri za mumewe, maana walipofika hotelini walioga tofauti tofauti, na hata mkaka alivyompandia mkewe,yule mdada alikuwa amelalia mgongo, hivyo hakuona kitu zaidi ya kuhisi tu)

    Basi yule mwanamke akavua taulo lake na kuweka kando, naam akabaki kama alivyozaliwa...na taratibu kabisa akamsogelea mumewe na kuanza kufungua ile kamba ya pajama taratibu, na alipoifungua akaanza kuivua/kuifunua hapo akiwa na macho ya hamu na woga, anagalau aone miliki yake laivu kwa macho yake, mara alivyofunua tu hivi na kumwacha mumewe Uchi kabisa....Binti alishtuka kwa mshangao na kusema "Mamaaaa" na hapo akaangukia kitandani na kuzimia......................ITAENDELEA!!!!


(Nini alichokiona mpaka ashtuke na kuzimia? Je nini kiliendelea baada ya hapo?...Usikose kufuatilia sehemu ya 4 ya ushuhuda huu wenye kukusaidia wewe msomaji kama utazingatia kwa makini)


@Kwa hisani kubwa ya http://quality-love.blogspot.com/ (c)2013
King Chavala-MC
+255 713 883 797