Saturday, January 4, 2014

.........UPENDO !!!!


(Jua uhusiano kati ya UASI kwenye MAHUSIANO ya kijamii na UPENDO wako kwa Mungu)

Ukifuatilia nyakati katika maandiko utagundua kwamba tunaishi nyakati za mwisho. Tumekaribia mahali ambapo Yesu anarudi kulichukua Kanisa lake. Hakuna ajuaye ni karibu kiasi gani ila ni KARIBU. Yesu anasema yuko malangoni, anakuja.

Yesu alisema dalili ya nyakati za mwisho (Mathayo 24:3-13) na zinaonekana. Ila nataka niongelee MAASI. Huku mwisho wa nyakati tuliko tunaambiwa KUTAONGEZEKA MAASI na UPENDO wa wengi utapoa. Upendo ni kitu cha ajabu sana ambacho Mungu amewaumbia wanadamu. Mtu AKIPENDA ghafla! anakua mtu wa hatari maana huo UPENDO utamsukuma kufanya vitu bila kujali “sana” GHARAMA wala MUDA. Kwa mfano UPENDO wa mtu kwa Mungu utamsukuma huyo mtu kusimama kwa UAMINIFU mbele za Mungu hata kama anateseka na ataridhika na kila kitu kigumu na cha MAUMIVU alimradi asimtende Mungu dhambi. Sasa, UPENDO wa mtu huyu UKIPOA hutaamini vitu ataanza kufanya. Ghafla! visingizio vingi sana vinaibuka na sababu nyingi sana za MSINGI za kumkosea Mungu zinaibuka, ila ukifuatilia kinachotokea kwa huyu ndugu ni kitu kimoja tu UPENDO WAKE KWA MUNGU UMEPOA!

Sasa tunajua kabisa kwamba Mungu wetu ana NGUVU kuliko Ibilisi. Na hakuna siku ibilisi atakinga MSULI kwa Yesu akafanikiwa maana Yesu yuko juu sana katika UWEZA, sana sana ikiibuka vita atamtuma tu MIKAELI akamshughulikie huko na yeye akaendelea kumtizama BIBI ARUSI wake anayempenda sana ambaye ni KANISA. Ibilisi anachofanya hapa kwa wana wa Mungu ni KUONGEZA MAASI kati yao! USALITI katika mahusiano, biashara, familia, ndugu, huduma, nk. Huu usaliti unasababisha watu KUJERUHIWA ndani yao na UPENDO wao UNAPOA bila wao kujua! Wengi sana wamefika mahali pa gumu sana na wameweka SILAHA zao chini kwa sababu wamejeruhuwa na ADUI wakiwa KAZINI. Madhara yake yanapelekea KAZI yao kusimama shambani mwa Bwana, wamebaki KULAUMIANA na SHUHUDA MFU za watu waliowatendea mambo “mabaya” badala ya kushuhudia MATENDO makuu ya Mungu!

Watumishi wengi sana na wana wa Mungu wameacha zile SHUHUDA za “kuokoa” watu na Ibilisi ameanza kuwatumia kusambaza shuhuda KANDAMIZI za kurudisha watu nyuma! Ushuhuda ni habari NJEMA! Hili ndilo jina jingine la INJILI, habari njema kwa watu wote! Sasa, watu wengi sana wamewekeza kwenye habari MBAYA za watu na zimewavunja wengi sana moyo (hasa wachanga katika imani) na kuwajeruhi badala ya kuwajenga! Hayo MAASI ambayo yametokea, na WEWE mwana wa Mungu umejeruhiwa na umepata UCHUNGU na kwasababu hujashughulikia uchungu wako UMENAJISI wengi kanisani na madhara ya ule UASI “mmoja” umekua JANGA kubwa maana umesambaa na KUZIMISHA upendo wa WENGI kwa mara moja bila wewe kujua. Tunaonywa tuangalie “shina la UCHUNGU lisichipuke ndani yetu” maana UCHUNGU ndani ya mtu mmoja una uwezo wa kunajisi watu WENGI ambao hawakuhusika katika TUKIO lililosababisha huo uchungu. Chunga sana hili ENEO maana unaweza kujikuta umegeuka kuwa mtumishi wa Ibilisi kusambaza UCHUNGU bila kujua na ukamfanikishia Ibilisi kazi yake ya KUNAJISI watu!

Nitatoa mfano wa huduma ya Yesu. Wakati huduma ya INJILI inaendelea kwa kasi kubwa, Petro na wenzake “wako tayari kupigana kwa upanga kumtetea Yesu hadi kufa”, na ikafika mahali Petro anatoa upanga ALANI mwake kwa ajili ya kumlinda Yesu, na alijikuta anakata mtu sikio ghafla, aliona huyu jamaa anamsogelea Yesu. UPENDO kwa Bwana wake ukamsukuma “kupiga mtu”. Kabla Petro hajakaa sawa anaona YUDA, ambaye ni MTUMISHI mwenzake hapo pembeni anachukua RUSHWA, kabla hajakaa sawa anaona ANAMBUSU Yesu hadharani, kabla hajakaa sawa anaona Bwana wake AMESALITIWA LIVE na sasa ANASULUBIWA! Na aliyemsaliti ni MTUMISHI mwenzake ambaye wamefanya HUDUMA pamoja kwa takriban mika 3! Yesu alimwamini YUDA kiasi cha kumfanya MWEKA HAZINA wa HUDUMA yao. Leo machoni pa kila mmoja wao katika HUDUMA na wakiwa KAZINI anamsaliti Bwana wao! Hili jambo liliwasambaratisha wote wakatawanyika, sio kwa hofu tu ya wale waliokua wanamsulubu Yesu lakini pia ile hali ya UASI iliyojitokeza imeathiri UPENDO wao na WAKARUDI nyuma!

Kabla Petro hajakaa sawa anaulizwa “wewe si ulikua na huyu jamaa”, Petro anasema SIMJUI mtu huyu! Hataki hata kutaja jina la Yesu, safari hii anamwita “mtu huyu”! Mara tatu anamkana YESU hadharani! ila kilichotokea kabla ya hapo ni UASI mkuu na USALITI wa waziwazi! Wanafunzi walitawanyika kwa sababu “mchungaji wao amepigwa”. Petro akarudi zake KUVUA samaki ziwani, akaachana na BIASHARA ya Yesu maana UPENDO umepoa! Huyu ni Yule Petro ambaye alisema “hata wakikuacha wote mimi sitakuacha, niko tayari kufa kwa ajili yako, nk”. Sasa kimetokea nini? Upendo umepoa. Yesu alipofufuka akamtafuta tena Petro, akamuuliza “Petro UNANIPENDA?”, akarudia mara ya pili “Petro UNANIPENDA?” na mara ya tatu kurudia Petro AKALIA! Na akamwambia “Bwana unajua nakupenda…”. Ninachotaka uone hapa ni ile hali ya KUKATA TAMAA na KURUDI nyuma ya Petro baada ya VURUGU nyingi kutokea katika HUDUMA yao. Na YESU alikua ANAHUISHA ule UPENDO kati yao ambao ULIATHIRIKA. Hapo wakati Yesu anampa Petro kazi unaweza kujiuliza kwanini amuulize kwanza “unanipenda” ndio asema “LISHA KONDOO”, “CHUNGA KONDOO”, nk.? Sababu ya msingi hapa ni HUWEZI kufanya kazi ya MUNGU kama HUMPENDI! Jaribu uone halafu mbwa mwitu aje kama hujakimbia na kuacha KONDOO wanaliwa huko! Nakwambia mchungaji ANAYEPENDA kondoo zake “itamgharimu” maisha kwa kondoo hao. Sio mimi, ni maandiko yamesema.

Sasa katika maisha ya leo wengi wetu tumejeruhiwa sana na “watu” katika michakato mbalimbali ya maisha na kwa sababu UASI umeongezeka UPENDO wetu kwa Mungu na kwa “hao watu” umeathirika kwa viwango tofauti. Wengine WAMEACHA wokovu na wengine WAMERUDI nyuma. Sasa Ibilisi akifanikiwa kukurudisha nyuma, ukampa nafasi ya kurudi pale alikofukuzwa wakati unampokea Yesu, huwa anaongeza “idadi ya MAPEPO mara 7, tena wale waovu zaidi, na hali ya mtu huyu inakua mbaya kuliko ya mwanzo”! ili akifanikiwa “akuchinje” kabisa usije ukatubu!

Ukifahamu SIRI hii utagundua ni kwanini MTU akisalitiwa katika MAHUSIANO ni rahisi sana kurudi nyuma katika WOKOVU pia! Ule UASI una NGUVU ya KUPOOZA upendo wako kwa Mungu na kukumaliza kiroho USIPOANGALIA. Katika NDOA, HUDUMA, MAKANISANI, nk. kumekua na hiki kitu cha KUSALITIANA na kimeathiri kazi ya Mungu kwa kiwango kikubwa sana kwa sababu kimegusa eneo nyeti la UPENDO. Ni jambo la kusikitisha sana “mmoja” katika HUDUMA au NDOA anakua AGENT wa shetani “kwa muda” (bila kujua) kama ilivyokua kwa YUDA. Na kwa kipindi kifupi anatumika kufanya KITU ambacho kitasambaratisha HUDUMA au NDOA moja kwa moja. Ibilisi akimwachia huyu mtu (kwa maana ilikua kwa kitambo tu) akizinduka, anajuta! Ndio maana YUDA alikimbilia KITANZI na wala ile RUSHWA hakuila! Alisikia vibaya sana baada ya KUFANYA ule UASI na USALITI na akachukua ile HELA na kuirudisha kwa wenyewe! Too LATE! Yesu yuko msalabani saa hizo na huku huduma ishasambaratika WATUMISHI wenzake akina Petro nao “washaharibu” na akina Yohana na wenzake washatokomea kusikojulikana. Yesu alipofufuka alifanya kazi ya KUWAKUSANYA hawa wanafunzi wake kwa UPYA baada ya kusambaratika vibaya.

Angalia mambo ya kwanza uyape umuhimu wa kwanza. Watu wengi sana wako busy na HUDUMA na kusahau kwamba UPENDO ni msingi wa YOTE. Mungu havutiwi sana na hayo mambo kama HUMPENDI, na utakosa Ufalme wa Mungu usipojipanga pamoja na huduma yako kubwa nchi nzima au hata dunia nzima. Kumbuka (1 Wakorintho 13:1,2) “Tena nijapokuwa na UNABII, na kujua SIRI zote na MAARIFA yote, nijapokuwa na IMANI TIMILIFU kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina UPENDO, si kitu mimi. 2 Tena NIKITOA MALI ZANGU ZOTE kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.” Shughulikia eneo lako la UPENDO wa KWANZA na Yesu. Fanya “toba” ya dhati ukikiri (kutaja kwa jina) pale “ulipoa anguka” maana unatakiwa UPAKUMBUKE na kumwambia Yesu, na kisha omba “maombi” yako ya dhati ili KUHUISHA ule UPENDO wa kwanza, na utaona mabadiliko na BARAKA zikimiminika kwako kwa namna ya tofauti.

Lengo la somo hili ni kukutahadharisha kuwa tuko nyakati za hatari. UASI ni mwingi na usipoangalia unaweza KUPOOZA UPENDO wako wa KWANZA! Na Yesu anasema na wewe akijua “umeuacha ule UPENDO wako wa kwanza”, ule ambao ulikuweka chini ukasoma Neno na kuomba na KUSHUHUDIA au kumtumikia Mungu katika ngazi mbali mbali. Naye anasema “kumbuka ni wapi ulipoanguka ukatubu”. Fanya HARAKA kwa sababu hizo njia za YUDA kweli zitakupa HELA, ila ni vipande 30 tu! Kumbuka thamani ya DAMU ya Yesu iliyokununua, FANYA uamuzi LEO kama UNAZIDI kumsaliti MWANA wa MUNGU au unamrudia. Mungu atusaidie kufanya maamuzi sahihi. NEEMA ya BWANA na iwe JUU yako tangu SASA na hata milele. AMEN.

Frank Philip.

Tuesday, October 29, 2013

HATIMAYE SAMUEL SASALI a.k.a Ze Blogger AU PAPAA SEBENE, MC NA MTANGAZAJI WA CHOMOZA YA CLOUDS TV AMEPATA MKE!!!

CHEREKOOOO CHEREKOOOOO.......

CERTIFIED MR SAMUEL AND MRS MILEMBE SASALI
SASA HAWA NI MUME NA MKE RASMI NA HIVYO NDIO VYETI VYAO VYA NDOA!!
NA HIYO HATUA HAPO JUU ILIFIKA BAADA TU YA KIAPO CHA KILA MMOJA KWA MWENZAKE PAMOJA NA PETE YA AHADI YA NDOA NA KUTUNZA KIAPO HICHO
 VAA PETE HII,IWE ISHARA YA AGANO LANGU KWAKO.....
 VAA PETE HII.....
GROOM'S MEN PAMOJA NA SAMUEL SASALI

MAIDS KUMPAMBA MILEMBE
KULIKUWEPO GROOM'S MEN NA MAIDS 30 KUIPAMBA HARUSI HII YA PAPAA SEBENE!
WALIINGIA KWA FURAHA SANA NA KILA MMOJA ALIFURAHIA UCHANGAMFU WAO

MR SAMUEL AKIONGEA NA KUMSIFIA MKEWE
MRS MILEMBE MADAHA WA SAMUEL AKIONGEA
TUKAPATA KUSIKIA SAUTI ZAO,WAKASEMA NA HATIMAYE WAKAPUMZIKA KIDOGO KABLA YA KUANZA ZOEZI LA KEKI!
MR & MRS SAMUEL AND MILEMBE SASALI
HATIMAYE WALIKATA KEKI NA KULA NA

KIPEKEE WALITOA ZAWADI YA KEKI KWA WATU WAO KADHAA MUHIMU SANA, AMBAO WAMEKUWA MSAADA KWA KILA MMOJA WAO NA KWA MAHUSIANO YAO.....BAADHI YA WALIOPEWA ZAWADI YA KEKI NI PAMOJA NA WAZAZI WA PANDE ZOTE MBILI,
 MILEMBE ALIPELEKA UKWENI...
NA HUKU PIA VIVYO HIVYO!

KAMATI YA MAANDALIZI,MARAFIKI HURU,AFLEWO TEAM,DK PARVINA,PROSPER MWAKITALIMA,APOSTLE ONESMO NDEGI, LINDA TEMBA NA DK.HURUMA NKONE, MCHUNGAJI ALIYEFUNGISHA NDOA HIYO!!
KEKI KWA MCHUNGAJI NA MKE WAKE

KEKI KWA PROSPER MWAKITALIMA

KEKI KWA DK PARVINA
HATIMAYE WATU WALIKUJA KUMPONGEZA KWA KUCHEZA NA KUMRUSHA JUU SANA...
NA BAADA YA HAPO MENGI YALIENDELEA,KAMA VILE KUONA SHORT DOCUMENTARY NA HATIMAYE CHAKULA,NA HAPO WALITUMBUIZA THE VOICE,SAMWEL YONAH, AMANI KAPAMA, BOMBY JOHNSON PAMOJA NA KING CHAVALA-MC NA KIBAO MAALUM KABISA KWA MAHARUSI "SAMILEMBE"
KING CHAVALA-MC
WATU WALIKUWA WAKITOA ZAWADI MLANGONI,LAKINI KUNA BAADHI YA WATU AU MAKUNDI MAALUM YALILAZIMIKA KUPELEKA MBELE ZAWADI ZAO.
KAMATI YA MAANDALIZI ILIENDA MBELE KWA KUCHEZA KAMA HIVI
CHRISTIAN BLOGGERS NAO HAWAKUBAKI NYUMA KATIKA KUMPONGEZA MWENZAO!
"SAMILEMBE"

HATIMAYE BAADA YA YOTE WALIPIGA PICHA NA KUONDOKA KUELEKEA HUKO AMBAKO HAKUNA AJUAYE NA WAO HUJUA TU WAKISHARUDI!!

SHUKRANI NYINGI SANA KWA KAMATI YA MAANDALIZI  NA KILA ALIYEHUSIKA KWA NAMNA MOJA AMA NYINGINE KUFANIKISHA JAMBO HILI,AHSANTE SANA MWENYEKITI NOEL TENGA KWA KUKUBALI KUTUMIKA KUBEBA JUKUMU HILI!

KWA NIABA YA TIMU NZIMA CHA YA CHAVALA MEDIA, TUNAWATAKIA KILA LAKHERI NA MAISHA MAREFU SANA YENYE FURAHA NA AMANI NA UPENDO WA KWELI WATU HAWA MUHIMU SANA KWETU,AMEN!!

IMEANDIKWA NA 
King Chavala MC
+255 713 883 797

Monday, September 30, 2013

Ladies of Destiny Network Presents "HOW TO CONTROL SPENDING"

n

NA UPENDO WA KWELI NDIO HUU....KUWA SEHEMU YA IBAADA YA KUSIFU NA KUABUDU TAR 06/10/2013 NA JOHN LISU!!

UKO HAPA DVD LIVE RECORDING
 NA JOHN LISSU,
06/10/2013,CCC-UPANGA, DAR ES SALAAM, TANZANIA.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA WATANZANIA WOTE;
SALAM TANZANIA!

Shalom Dar es salaam, Shalom Tanzania!
Ndugu wanahabari na watanzania wote kwa ujumla!
Naamini tuko salama na tunaendelea na shughuli zetu za kila siku alizotupatia Mungu wa mbinguni, tumshukuru Mungu sana kwa Amani na utulivu aliotupa na tuendelee kumuomba ili atuepushe na kila aina ya dhahama na uharibifu wa Yule adui!
Kama tulivyosikia hivi karibuni, yale yaliyotokea nchi jirani ya Kenya, kwa hakika tunawapa pole sana kwa mkasa huo, pole kwa wale waliowapoteza wapendwa wao na wale waliojeruhika tunawaombea wapone haraka, tunaamini hekima ya Mungu itakuwa juu ya serikali yao kushughulikia jambo hilo kikamilifu.
Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai, hata sasa tunapoende kumalizia robo ya tatu ya mwaka 2013, tumeshuhudia mambo mengi sana mwaka huu ya kila aina, yapo yale yalionza kwa mara ya kwanza na mengine yamekuwa ni mwendelezo tu wa yale yadumuyo au yalioyaanza hapo kale, tumeshuhudia michezo mbalimbali na vipaji lukuki vikiinuka na kuimarika katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu, na kwa yote mema na mazuri tunampa Mungu Utukufu kwa hakika!


UTANGULIZI JUU YA JOHN LISU;

John Lisu ni mmoja wa waimbaji/Waabudishaji wanaoheshimika katika Tasnia ya muziki wa Injili kutokana na mchango wake mkubwa alioutoa katika kukuza na kuendeleza muziki wa Injili nchini Tanzania na nje ya Nchi. Nyimbo nyingi alizozitunga na kuziimba zimekuwa zikitumika katika makanisa mbalimbali kama nyimbo za kusifu na kuabudu; pia waimbaji wengine waliokua wakiimba naye wameweza kukua na kufikia uwezo wa kuwa waimbaji wa kujitegemea. John Lisu pia ametia hamasa kubwa miongoni wa wanamuziki wa Injili kuanza kufanya muziki wa live. John Lisu ameweza kufanya tours za ndani ya Tanzania, Africa na Bara la Ulaya kwa ajili ya huduma.
CHRISTINA SHUSHO

John Lisu anategemea kufanya Project II ya Live recoding inayojulikana kama "UKO HAPA" baada ya project ya kwanza ya Jehova yu hai kufanya vizuri sana. Tamasha litafanyika ndani ya ukumbi wa City Christian Centre (CCC) Upanga tarehe 6 Octoba 2013, kuanzia saa 8. mpaka saa 2 usiku.
PAUL CLEMENT

 Tamasha litasindikizwa na waimbaji nguli kama Christina Shusho, Neema Gospel Choir, Paul Clement, Pastor Safari Paul, Bomby Johnson Waimbaji wote wamethibitisha kuwepo. 

BOMBY JOHNSON

VENUE:
City Christian Centre (CCC) mkabala na chuo kikuu cha mzumbe
Si mbali saana kutoka Diamond Jubilee
MIRIUM LUKINDO WA MAUKI


USAFIRI (basi zilizobandikwa matangazo ya tamasha) utakuwepo kutoka posta mpya kwenda ukumbini kuanzia saa saba na nusu mchana kwa bei ya kawaida.
PASTOR SAFARI PAUL

HABARI NJEMA-MUHTSARI!!!!!

Sasa kwa mara pili nchini Tanzania, mwimbaji WA NYIMBO ZA INJILI na mwabuduji JOHN LISSU wa jijini Dar Es Salaam, atakuwa anafanya Ibaada kubwa ama Tamasha la kusifu la Kuabudu(LIVE PERFORMANCE), litakalorekodiwa moja kwa moja (DVD LIVE RECORDING) lenye jina “UKO HAPA” (Yaani Mungu na Uwepo wake).
Tamasha hilo litafanyika jumapili ya Tarehe 6, Octoba 2013  katika Ukumbi mkubwa wa kisasa wa Kanisa la City Christian Centre (CCC)- Upanga, mkabala na Chuo Kikuu Mzumbe – tawi la Dar es salaam, kuanzia saa nane mchana.
Tunataraji watu 5000 kuwa sehemu ya tamasha hili la kipekee,Utakuwa sehemu ya tamasha hilo kwa tiketi ya 10,000/= (kawaida), 20,000/= (VIP) na 3000/= (Watoto);
na Kwale watakaohitaji tisheti maalum za tukio hilo, basi zinapatikana kwa kati ya 12,000-15,000/=, wewe wasiliana tu na (0713905118)
NELLY-MKE WA JOHN LISU


VITUO VYA KUUZIA TIKETI;
1.   MWENGE – Tarakea duka la Kanda
2.   KINONDONI – DPC
3.   MLIMANICITY – Silverspoon Restaurant
4.   KARIAKOO – Mbogo Shop
5.   UKONGA BANANA – KWA GIDO
6.   POSTA - DUKA LA MSAMA

T-SHIRTS

-T-shirts maalumu kwa wanaume na wanawake zinapatikana katika vituo vya kuuzia tiketi kwa bei ya elfu kumi, mpaka elfu 15(kutegmeana na aina).

N.B; Kwa tiketi ya VIP, mnunuzi atajipatia na Audio CD ya John Lissu ya “Uko Hapa”

USAFIRI UTAKUWEPO!!
Siku ya tamasha kutakuwepo usafiri kutoka Posta Mpya mpaka CCC-Upanga,eneo la tukio, hivyo kama wewe ni mgeni na hupafahamu mahali hapo, basi utakachotakiwa kufanya ni kupanda magari toka ulipo mpaka posta mpya kabla ya saa nane,na hapo utayakuta mabasi yenye mabango ya Tamasha, basi utajongea humo na hapo utawezeshwa kufika eneo la tukio, muhimu ni kuzingatia muda!

MUHIMU SANA!!

JOHN LISU NA TIMU NZIMA WAKIWA MAZOEZINI


Tamasha hili ni muhimu sana kwa Tanzania, hasa ukizingatia JOHN LISSU ni mmoja wa waimbaji wa kwanza kuimba live kila mahali anapoalikwa na ni mwimbaji wa kwanza binafsi kufanya LIVE DVD RECORDING pale Ubungo plaza, na ile ya kwanza iliitwa “JEHOVA YU HAI” na sasa anafanya LIVE RECORDING kwa viwango vingine bora zaidi, maana Mungu hutupa hatua moja zaidi kila siku.
Ni muhimu kwa kila mtanzania kujivunia kipaji na tukio hili muhimu katika historia, njoo umwabudu na kumsifu Mungu pamoja, Njoo ujifunze, Njoo umuunge mkono mtanzania mwenzako na njoo uje ufanyike sehemu ya Historia hii kwa Utukufu wa Jehova.
NEEMA GOSPEL CHOIR-KWAYA PEKEE ITAKAYOSHIRIKI "UKO HAPA"


MWALIKO MAALUM;
Kipekee Ninapenda kuwakaribisha wachungaji, mitume, manabii, wainjilisti, waalimu na viongozi wote wa makanisa na huduma mbalimbali, ninawakaribisha viongozi wote wa kisiasa na kijamii kutoka serikalini na vyama vya siasa vyote, ninapenda kuwakaribisha wanaharakati na wanataaluma wote, ninapenda kuwakaribisha waimbaji wote wa nyimbo za injili na wanasanaa wote, ninapenda kuwakaribisa wanafamilia wote, asiwepo wa kubaki nyuma, ninapenda sasa kukukaribisha wewe unaesoma hapa, naam nisaidie kumkaribisha na mwenzako na yeye aje na mwenzake, kimsingi tukio hili ni letu wote bila kujali kitu chochote, njooni tumsifu na kumwabudu Bwana na Mungu hataacha kuibariki Tanzania!
EMMANUEL NDIYE ATAKAYEMPIGIA JOHN LISU LEADING GUITOR


SHUKRANI;
Tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa Hakneel Production (Wadhamini wakuu), na Jonn Lissu na timu nzima ya maandalizi; Kanisa la CCC-Upanga; vyombo vya habari hususani Praise Power na WAPO Radio; Clouds TV kupitia CHOMOZA na Clouds Radio kupitia GT; Sibuka Tv kupita Gospel Hits; Bloggers hususani Christian Bloggers, magazeti na vyombo vingine vyote vya habari! Shukrani hizi zimfikie kila mtu mmoja mmoja aliyetoa mchango wa mawazo, fedha, ushauri, maombi, ubunifu, yaani mchango wowote wa hali na mali na Mungu awabariki nyote!
MIRIUM LUKINDO WA MAUKI


MUHTASARI MKUU;
Tukio; TAMASHA LA KUSIFU NA KUABUDU, LITAKALOREKODIWA
(DVD LIVE RECORDING CONCERT)
Mhusika; JOHN LISSU
Jina: “UKO HAPA”
Mahali; UKUMBI WA KANISA LA CITY CHRISTIAN CENTRE (CCC)- UPANGA
Lini; 06TH OCTOBA, 2013
Muda; KUANZIA SAA NANE MCHANA
Kiingilio; Tsh 10,000/= (kawaida); 20,000/= (VIP) na 5000/= (Watoto)

Wasindikizaji; CHRISTINA SHUSHO, MIRIUM LUKINDO, PASTOR SAFARI, BOMBY JOHNSON, NEEMA GOSPEL CHOIR-AIC Chang’ombe na PAUL CLEMENT.

Mengineyo; USAFIRI UTAKUWEPO TOKA POSTA MPAKA CCC-UPANGA na Unaweza kujipatia Tisheti pia.
Wahusika; WATU WOTE MNAKARIBISHWA!


UKIPATA HABARI HII USIACHE KUMSHIRIKISHA NA MWENZAKO, NAAMINI HAUTAKOSA TUKIO HILI MUHIMU LA KIHISTORIA KATIKA NCHI YA TANZANIA KWA UTUKUFU WA MUNGU!!





KWA PICHA NA TAARIFA ZAIDI;


http://www.youtube.com/watch?feature=player_detailpage&v=blz0PKQ6QNU




MAWASILIANO:
O713 240 397 – JOHN LISU
0713 905 118 –PROSPER MWAKITALIMA – EVENT MANAGER
0713 883 797 - FREDY CHAVALA - PUBLICITY


Imetolewa na;
Fredy E. Chavala <King Chavala (MC)>
Publicity Manager
+255 713 883 797
On Behalf of The Organizing Committee

Wednesday, September 18, 2013

PASTOR FRED AND NEEMA OKELLO'S WEDDING IN PICTURES!!!


 PASTOR CHRIS OFFICIATING THE WEDDING OF FRED AND NEEMA....AND PASTOR MABINA ASIDE!
 ....VAA PETE HII
 .......NOW LET US GO TO SIGN!
 .......THIS IS THE CERTIFICATE TO SHOW THAT NOW WE ARE HUSBAND AND WIFE!
 .....WITH MAIDS!
 .....WITH PARENTS OF BOTH SIDES!
 .....FRIENDS FROM TANZANIA IN UGANDA!
 .....FRIENDS FROM TZ WITH FRED AND NEEMA!
 .....A VERY BEAUTIFUL CAKE!
 ....A VERY NICE VIEW  OF FRED AND NEEMA'S RECEPTION ALONG LAKE VICTORIA
 .....PARENTS OF FRED

 .....CUTTING OF A CAKE!
 .....A VERY SPECIAL MLISHANO OF CAKE!
 ......KUNYWA MUME WANGU!
MR AND MRS FRED AND NEEMA OKELLO