Monday, August 12, 2013

USIKU ULE WA KWANZA WA FUNGATE (HONEYMOON).........Part 4!!!



Hello rafiki habari yako!
Naamini umekuwa unafuatilia sana habari hii
Iliyoanzia hapa



SAWASAWA NA Wafilipi 4:8...."Hatimaye ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa njema, ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote,yatafakarini hayo."

NDIO NA MIMI NAWALETEA SIMULIZI HII ILI MWISHONI KWA PAMOJA TUTAFAKARI;

ILIPOISHIA PART 3;
....mara alivyofunua tu hivi na kumwacha mumewe Uchi kabisa....Binti alishtuka kwa mshangao na kusema "Mamaaaa" na hapo akaangukia kitandani na kuzimia...............

ENDELEA SASA NA PART 4; 
Na kwasababu mume wake alikuwa amepitiwa na usingizi wa kuchoka,hata uliposikika ule mshindo pamoja ile sauti ya “mamaaa”, mume wake hakusikia ila inahisika kuwa kuna watu walisikia chumba kingine na hivyo wakaamua kugiga simu mapokezi na kuwatarifu wahudumu wa Hotel, na hiyo iliwalazimu wahudumu wa Hotel kugonga vyumba kadhaa ili kujua hasa ni wapi ilikuwepo shida….na walipogonga chumba No 307, basi toka usingizini Yule mtumishi akashtuka kwa nguvu na kuona mke wake amelala uchi kabisa tena sio kulala kivile ni kama amejibwaga tu,basi akamfunika haraka na kwenda kusikia anayegonga mlango……na alipofungua akashangaa kuulizwa kuna shida gani humu mbona kuna sauti ya mshtuko imesikika huku? Basi haraka akajibu mke wangu huwa anashtuka shtuka hata akiona mende tu, sasa yamkini kuna jambo limeshtua,ila hakuna tatizo lolote lile na kama ikiwepo shida nitawapigia simu,samahani sana kwa usumbufu….basi wale wahudumu wa hotel  wakaondoka lakini kwa shingo upande, naye akafunga mlango na kurudi ndani.

Aliporejea akawa na maswali mengi sana kichwani maana hata hakujua nini kimetokea na basi alichokifanya ni kumbeba mke wake na kumlaza vizuri kitandani….na akamlaza akiwa anatazama juu,basi kabla hajamfunika alibaki kwa sekunde kadhaa akiwa anamshangaa Mungu kwa uumbaji wa mke wake….na baada ya muda akawa ameshikwa na haja ndogo basi akakimbia mara moja chooni, na alipofika huko kwanza akashtuka sana kuwa ile pajama yake ilikuwa wazi, I mean ilikuwa imefungunguliwa na hapo akapata kigugumizi cha kuwaza…ina maana na wale wahudumu wawili wa hoteli walimuona utupu wake? Lakini hakufungua mlango wote wa chumbani mmmh yamkini hawajaona kitu….na alipotaka kukojoa akagundua kuna upungufu Fulani anao,basi akamaliza haraka na kunawa mikono na kurudi haraka na kuanza kuangalia huku na kule na kumbe ilikuwa chini ya kitanda na ilianguka pale alipostuka kwa nguvu wakati mlango wa chumba cha hoteli kikigongwa na hapo akaokota na kuweka kwenye droo ya kitanda chake, na hapo akawaza zaidi ina maana mke wangu ameona?

Basi akiwa na mikono mibichi akawa amemshika usoni kwa namna ya kumfuta machozi na kupitisha mikono mwilini mwake kwa namna ya kubembeleza na muda wote huo asijue ya kuwa mke wake amezimia na hapo akidhani mke wake amelala…..kwasababu ya ubaridi wa mikono ile na Uwezo wa Mungu tu Yule binti akashtuka na kuanza kulia….Jamani hivyo ndio nini? Maana yake nini sasa? Sitaki….sitaki……sitaki…… na kuendelea kulia kwa huzuni, basi huyu mtumishi akashangaa na kuendelea kumbembeleza jamani basi yanazungumzika…..kwa akili ya kawaida Yule mtumishi alidhani mke wake analalamikia Afro ambayo alikuwa nayo kichwani pamoja na ikulu,tena zote zilikuwa zimesheheni na zilikuwa zimetunzwa vizuri….kwa haraka unaweza ukasema labda ni nadhiri ya Bwana ya utumishi kama ya Samson, kwamba asinyoe mpaka hapo kusudi la Bwana litakalotimilika.

Yule dada akanyamaza bila kuongea zaidi nae akawa amekaa pale kitandani kwa kuwaza san asana na mume wake alikuwa ameshalala zamani sana,yaani ule usingizi wa pono, basi Yule dada akaamka na kukaa kitandani asijue afanye nini….Je aombe? Je awaambie wasimamizi wa ndoa? Au amtaarifu mama yake?....Basi akajiambia moyoni ngoja nione tena ili athibitishe kuwa alikuwa anaota au laah!
Basi taratibu akaifungua tena ile kamba ya pajama ya mume wake na kufunua taratibu, na saa alichokiona ni tofauti….”Mmmmmh!” aliguna kwa mshtuko na hapo akapata ujasiri akaingiza mkono na kupapasa,na hapo alibaki ameduwaa na hapo akawa na maswali mengi zaidi ya majibu…..mbona alichokiona hapo kwanza hakifanani na hiki,au hii ndio miujiza ya mtumishi wa Bwana,oooh hapana hakuweza kuvumilia,akamfunika bila kufunga vile kamba ilivyokuwa,akaamka na kuoga haraka na kuvaa jinsi yake na tisheti na kuchukua simu yake,pochi na vile vitu vyake vya muhimu tu na kuacha vingine vyote hapo ndani kama vile shela ya harusi na zawadi zote alizokuwa ameletewa…..na hapo akaandika ujumbe kwa mume wake na kuacha mezani na kuandika ujumbe wa simu kwa mama na wasimamizi wa harusi na kisha akaitoa ile kadi ya simu na kuitumbukiza chooni,ili asiwepo mtu wa kumtafuta…na hapo akabeba kijibegi chake, na kufungua mlango taratibu na kufanya manuva pale mapokezi na getini kwa mlinzi na kuishia zake na hiyo ilikuwa mida ya saa kumi na moja na robo.


Huku nyuma mida ya saa kumi na mbili hivi huyu jamaa alishtuliwa simu zikiita mfululizo na alipoamka cha kwanza ni kuona mke hayupo na hivyo akaenda kuangalia chooni na bafuni, holaa…chini ya kitanda holaaa…basi katika hali ya kuchanganyikiwa akatoka na pajama mpaka mapokezi na wao wakasema hawajamuona mke wake hapo,ila kuna mkaka mmoja tu ametoka alikuwa anawahi safari yake, wasijue ya kuwa binti Yule alifungua mlango mmoja ulikuwa wazi wa chumba alichokuwapo kaka mmoja akiwa hoi amelala kama amekufa na kuchukua ufunguo wa hapo na kuwasilisha mapokezi na hawa wa mapokezi sababu ya usingizi na wao walisema uweke tu hapo mezani…….hivyo Yule mtumishi akachoka na kurudi chumbani kwake haraka,akiwaacha wahudumu wa hoteli pamoja na mlinzi wakizozana na meneja maana wamekuwa wazembe…..

Yule mtumishi aliporejea chumbani akaona simu yake ina miito mikoso (missed calls) zaidi ya hamsini toka kwa mama wa binti,wasimamizi wa harusi,wazazi wake pamoja na marafiki zake wa karibu waliotaka kujua kulikoni maana wengine waliifahamu siri, basi akiwa hajakaa sawa akaona kijikaratasi mezani na anapokifuata ili ajue kimeandikwa nini,mara mlango ukafunguliwa haraka na hapo wakaingia wasimamizi wa harusi yao pamoja na mzazi wa binti akifuata nyuma na hivyo akakichukua kile kikaratasi na kuficha katika mfuko wa pajama na kukaa kitandani kwa kuhamaki,asijue awajibu nini watu hawa wenye maswali mengi yaliyojaa hofu ambayo hata yeye mwenye we hana majibu yake……Basi wakiwa wanatmbea huku na huku na kuuliza swali hili na lile, mama mkwe alibaki tu akilia pembeni kwa huzuni.

Huku chini nako mzozo ulizidi na wale wahudumu wa hoteli wa zamu pamoja na mlinzi kazi ikaota manyasi, na hapo meneja akaja chumbani na kuanza kuomba radhi kwa yote yaliyotokea,alifanya hivyo kulinda hadhi ya hoteli yao na kulinda kibarua chake,lakini mle chumbani kila mmoja alikuwa na lake na sijui hata kama walikuwa wanamuelewa….basi kwa pamoja wote wakamwambia Usijali,ahsante kama tutahitaji ushahidi wowote ule tutakutaarifu,basi meneja akatoka na kuwaacha na wao wakabaki na kuongea kitumishi na kiutu uzima na baada ya mazungumzo ya kina kiasi,basi wote kwa pamoja wakaamua ku……………………………….ITAENDELEA!!!


(Usijaribu kutabiri watu hawa waliamua nini,maana hutajua mpaka nimekujuza. Naam…..Unataka kujua Binti huyo alienda wapi? Alionekana baada ya muda gani? Na alifanya nini aliporudi? Je unajua aliona nini na yeye kudhani ni mazingaombwe? Je nini hasa ukweli wa kile alichokiona na kuamua kuikimbia ndoa yake? Je kijana alifanya nini baada ya hapo? Kanisani alionekanaje? Kwa haya pamoja na USHAURI WA MWANDISHI sawasawa na Maandiko basi….Usikose sehemu ya 5 na ya mwisho ya hadithi hii yenye ukweli na mafunzo ndani yake, kwako wewe ambaye hujakutwa na dhahama ya namna hii, Ahsante kwa kufuatilia USIKU WA KWANZA WA FUNGATE!!

INALETWA KWENU NA;
KING CHAVALA-MC
+255 713 883 797
(c)2013

Tuesday, August 6, 2013

WATOTO YATIMA WA HOCET WANA UHITAJI WA CHAKULA MKUBWA SANA...SHOW LOVE PLEASE!!!!

SHALOM!
HABARI ZENU WAPENDWA!!
NINAAMINI MNA MOYO WA UPENDO, TENA WA KUWAJALI WENGINE KULIKO NINYI, NA HATA ZAIDI BIBLIA INASEMA UPENDO WA KWELI NI ULE WA KUWAPENDA WENGINE ZAIDI.
*****HANANASIFU ORPHANAGE CENTRE (HOCET)....HAWANA CHAKULA KABISAAAAA NA WEWE NA MIMI PEKEE NDIO TUNAWEZA KUWALISHA KWA SIKU 120, KABLA HAWAJAANZA KUJITEGEMEA****
LEO NINALO OMBI MAALUM KWENU, NI MUHIMU SANA SANA....KUNA KITUO KIMOJA CHA KULELEA WATOTO YATIMA (WATOTO WA MUNGU), KITUO KINACHOENDESHWA NA WATU TU WALIOJITOLEA, NA HAPO AWALI KILIKUWAQ KINAFADHILIWA NA WAZUNGU FULANI, LAKINI BAADA YA KUONA WATOTO HAO WAMEKAZANA NA MUNGU NA HAO WAZUNGU (WAFADHILI) WAKAWEKA MASHARTI, ETI KAMA WAKITAKA WAENDELEE KUPOKEA MISAADA YAO BASI WAACHANE NA HAYO MAMBO YA YESU YESU....NA KWA KUWA HAKUNA BABA MWINGINE ZAIDI YA MBINGUNI NA HAKUNA  NAMNA BINADAMU ANAWEZA KUISHI KWA MISAADA YA BINADAMU MWINGINE BAADA YA KUMKANA MUNGU WA KWELI.
 
SASA WATOTO HAO WAKO KWENYE ENEO LAO LA SHULE WANASOMA NA WANAYO MIRADI AMBAYO BADO HAIJAANZA KULETA FAIDA ILI WAWEZE KUJIENDESHA WENYEWE, NAHIYO ITAKUWA HIVYO TU BAADA YA MIEZI MITATU AU MINNE KUANZAIA SASA.
WATOTO HAWA KWA SASA HAWANA CHAKULA KABISA, NA HATA LEO WAMEKULA KWA MSAADA WA KIJANA MMOJA ALIJITOLEA YEYE BINAFSI NA FAMILIA YAKE....MBALI NA GHARAMA NYINGINE ZA UENDESHAJI KAMA MISHAHARA/POSHO ZA WALIMU;
************************************************************************************************
KITUO HIKI KINATUMIA UNGA KILO 30, MAHARAGE KILO 14 NA SUKARI KILO 5....NA IKIWA NI WALI,BASI HUHITAJIKA KILO 30 ZA MCHELE KWA MLO MMOJA....NA PIA UNAWEZA KUCHANGIA MAFUTA NA FEDHA KWA AJILI YA VITU VINGINE VINAVYOWEZA KUHITAJIKA.
************************************************************************************************

NINAAMINI KWA MSAADA WA WATANZANIA WOTE WENYE MAPENZI MEMA NA WATOTO WA KITANZANIA, WATOTO HAWA HAWATAKOSA CHAKULA KWA SIKU HIZI 120 ZA MPITO KABLA HAWAJAANZA KUJITEGEMEA WENYEWE, SIO LAZIMA ULETE MSAADA MKUBWA SANA, LAKINI NAAMINI UNAWEZA UKAJITOLEA CHAKULA KIASI JAPO KWA SIKU MOJA TU KAMA SIO TATU, YAWEZA KUWA WEWE BINAFSI AU KAMPUNI AU FAMILIA AU KANISA, LAKINI NINACHOKIAMINI NI KUWA KAMA KWELI TUNAAMINISHA KUMPENDA MUNGU NA KUWAPENDA WATOTO WATANZANIA TENA WANAOLELEWA KATIKA MALEZI YA KIMUNGU BASI LAZIMA WATOTO HAWA WATAISHI BILA HOFU YA CHAKULA KWA SIMU HIZI 120, NA KWA HAKIKA BWANA ATAKUBARIKI SAWASAWA NA IMANI YAKO KWAKE
YAK 1:27 "....DINI ILIYO SAFI ISIYO NA TAKA MBELE ZA MUNGUBABA NI HII, KUWATAZAMA WAJANE NA YATIMA KATIKA DHIKI YAO NA KUJILINDA NA DUNIA PASIPO NA MAWAA"
 
MSAADA HUO UNAHITAJIKA SANA SANA, NAAM KWA NAMNA YOYOTE ILE UNAYOWEZA KUCHANGIA BASI USISITE,FANYA HIVYO...SADAKA YAKO YA KUWALISHA WATOTO HAWA HAITASAHAULIKA HATA KIDOGO, UNAWEZA KULETA MCHANGO WAKO WA CHAKULA PALE OFISI ZA NIIM COMPUTERS, MOROCO HOTEL AU UKATUMA MCHANGO WAKO WA FEDHA KWA NJIA YA SIMU, NAAM KWA MAULIZO ZAIDI 
TAFADHALI WASILIANA NA WASIMAMIZI NA WARATIBU WA ZOEZI HILI KWA NO.
0713 26 1425 na 0754 527955, pia 0783 757051
KWA NIABA YA WASIMAMIZI WA KITUO HIKI NINAWASHUKURU HATA KABLA HAMJAFANYA JAMBO LOLOTE MAANA NAAMINI UMEGUSWA NA UKO TAYARI SASA KUWASAIDIA WATOTO HAWA...KAMA TUNAWEZA KUCHANGIA SHEREHE ZA HARUSI, NAFIKIRI HATMA YA WATOTO HAWA NI ZAIDI,MUNGU AKUBARIKI UNAPOMSHIRIKISHA NA MWENZAKO!!
 
Imeandikwa na
KING CHAVALA MC
KWA UDHAMINI MKUBWA WA CHAVALA IDEAS PLATFORM.

Monday, August 5, 2013

USIKU ULE WA KWANZA WA FUNGATE (HONEYMOON)- Part 3

Habari zenu ndugu wasomaji na wafuatiliaji wa Mkasa huu uliotokea mkoani Pwani,pale kibaha ambapo binti mmoja alimtoroka mume wake baada ya usiku mmoja tu wa honeymoon.

Tuliazia hapa...http://quality-love.blogspot.com/2013/06/usiku-ule-wa-kwanza-wa-fungatehoneymoon.html
 
habari zenu naamini mko wazima sana, na naamini bado unafuatilia habari hii ya binti huyu aliyetoroka usiku ule wa kwanza wa fungate....habari iwe chachu kwako kujifunza na kuzingatia mambo yale ambayo yamkini huyajui lakini yamewagharimu wenzako wengi na hata sasa ndoa zao zina shida....KARIBU SANA!!
 
ILIVYOISHIA Part 2. 
http://quality-love.blogspot.com/2013/07/usiku-ule-wa-kwanza-wa-fungate.html

.....na huku baada ya maombi ya mtumishi ya takribani masaa mawili, nae akaenda kuoga na kurudi akiwa na pajama na kumkuta mkewe amepitiwa na usingizi akiwa amelalia mgongo akiwa na Taulo tu, basi hivyohivyo Mtumishi huyo akaamua kum...........INAENDELEA HAPA CHINI!

NAJUA KILA MMOJA ALIKUWA NA HISIA NA MTAZAMO WAKE JUU YA WATU HAWA, BAADA YA KUJUA KWA SEHEMU KILE KILICHOTOKEA USIKU ULE...HAMNA UBAYA YALE YALIKUWA YAKO...ILA UKWELI MWENYEWE NI HUU.....ENDELEA!!

.....shtua kwa kumtikisa kidogo, huku akimwangalia kwa macho ambayo hata yeye mwenyewe alishindwa kuyaelezea; sijui ni macho ya huruma au kuombwa kuonewa huruma,sijui ni wivu au hasira au ndio macho ya mtumishi ya kuomba msamaha...basi yule mke alivyostuka kwa nguvu toka usingizini, akajigeuza kwa haraka na taulo lake likafunguka,hivyo akabaki kama alivyozaliwa....basi huyu kijana alibaki ameduwaa kana kwamba hajui kinachoendelea....akiwa mdomo wazi kwa takribani dakika moja na nusu hivi basi yule mrembo akawa macho kabisa na akawa nae anamshangaa mbona mume wake anamshangaa kana kwamba haamini ni yeye.

    Lazima ikumbukwe kuwa kijana huyu hajawahi kabisa kujihusisha na mambo ya mapenzi zaidi ya zamani zile za utoto wakati akidimba (Hii inadhihirishwa na matendo yake ya wazi kabisa ambayo hayategemewi kutokea Honeymoon)...lakini binti ana utalaamu wa kina kupita maelezo ya kawaida,maana ameshawahi kuruka ruka huko na kisha akarejea kundini, namaanisha akarudi wokovuni na ndio hapo akapata bahati ya kuolewa.

    Basi yule binti alipoona mume wake anamshangaa akaamka na kumvuta mkono kwa nguvu,hivyo yule jamaa akaangukia kifuani kwa mke wake, na hapo mke akamkaba shingo na kumparamia kana kwamba anapanda mti lakini mti ulioinama na hapo binti akawa anajaribu sarakasi zake za mahaba...lakini kijana hakuonekana na ushirikiano saaana japo alikuwa anaweza kujigeuza na kurudia maneno yale yale zaidi ya mara ishirini...."Unajua nakupenda sana Mke wangu"...basi kwa kuwa binti alikuwa na hasira hapo kwanza, nazo zikaisha zote...na mara baada ya binti kumuelekeza mumewe kuwa naomba nishike hapa na hapa, japo kwa woga na mshangao mtumishi akafanya hivyo...japo alibahatisha tu, inaonekana ile injini ya yule mwanamke ilikuwa "ON" na ilikuwa mtelemkoni, yaani alikuwa anasubiriwa mtu tu atoe kigogo uone linavyowaka.

(Samahani kwa lugha hii ngumu, na kama itakuwa kwazo kwa yeyote tusameheane ingawa naamini kila anayesoma hapa  ni mtu mzima na anaweza kuwa anaelewa....kimsingi ashiki ya kufanya mapenzi huanzia kichwani, kama kuna ule utayari na hamu basi ashiki hiyo hupandisha joto la hisia kwa haraka sana...na wakati wa tendo, wanaume hufika mwisho wa hatua moja na kuridhika ndani hata ya dk moja mpaka tano tu, lakini kwa wanawake inaweza kuwa mara tano zaidi ya wanaume...kwa hiyo kuna maandalizi yanapaswa kufanyika ili angalau safari ianzie mahali ambapo wote wawili hawatachelewa kufika. Na kama hawa wawili wakifika kwa pamoja basi jambo hili huwa ni jema sana kwa wote)

    Basi mara tu ya yule jamaa kukumbuka kuwa yeye ni mume wa mtu na kuna kitu anapaswa kufanya, alijigeuza haraka na sasa mwanamke akawa chini na yeye akawa juu...bila kujali mwanamke anaendelea na juhudi gani, na yeye akafungua kamba ya pajama yake na kutafuta mkao wa magoti vizuri, bila kusema neno lolote, kwa pupa na kwa haraka mtumishi  "AkaINGIA"....Na basi kwa sauti ya kulalamika yule dada akashtuka na akalia kiana akisema (Akataja jina) mbona hivyo jamani?...ni dhahiri kuwa alikuwa mtulivu kwa zaidi ya miaka miwili na saa hiyo ukavu ulikuwa upo wa kutosha na ndio maana alilalamika mmh...

     Ndoa ni uvumilivu, basi yule binti akajiachilia na kuchukulia ize na akaona sio sawa kumlalamikia mtumishi wa bwana, maana kwanza hana hakika kama anajua au laah! Basi yule mdada akiwa amemwachia mumewe aendelee na ibaada, huku akawa anafanya juhudi binafsi ili angalau akaribie, basi yule kijana alijisukuma kama mara kadhaa tu,haisemekani wala kuaminika kuwa ilipitiliza mara kumi, kijana akawa ameshamaliza ibaada na kutoa matoleo na kuganda kimya kwa muda kama zile zile video za You-tube zinavyogandaga kwa internet yenye kasi ya chini....hapo kijana alikuwa amekakamaa kama vile kuna kitu kinachofolewa mwilini mwake, lakini kama ujuavyo uzoefu mpya lazima mtumishi atokwe na jasho.

     Jambo la kushangaza, baada ya yeye kutoa matoleo, akafikiri na mkewe na ibaada ishaisha kumbe masikini ya mkewe iko taratibu na ndio kwanza ilikuwa inaanza kuchanganya, ikavurugwa na wakati inataka kurudi kwenye mwendo ule wa kawaida kurudi rahani, basi yule mtumishi Akachomoka na kujifuta kidogo na Taulo na kumfuta mkewe na kisha akafunga pajama yake na kulala kando ya mkewe...yule binti alibaki kushangaa tu....hasira za uchungu zikaanza kuja na hapo mrembo yuko ile heat ya juu kabisa, basi akamwambia mumewe azime taa ili angalau ajisaidie na kusogeza mbele ibaada japo mpaka wakati wa matoleo...mume akagoma akasema hapana tuiache tu....basi yule msicha akaamua kwenda bafuni na huko akajifungia na kuamua kujisogeza manualy mpaka akafika, japo ni dhambi na sio nzuri kihivyo, lakini anasema alifika.

    Alipomaliza akakaa sana huko bafuni na kulia sana, akijaribu kufikiri hivi kweli mume wangu ndio huyu na hii ni siku ya kwanza tu yuko hivi...maisha kweli yataenda....basi mawazo mengi yakawa yanazunguka kichwani....anakumbuka nasaha wakati wa kitchen party...anakumbuka mahosia ya baba na mama...tena anakumbuka ndugu na jamaa waliowahi kuvunjs ndoa...anajaribu kukumbuka mapenzi aliyowahi kufanya huko duniani na akichanganya na wale waliowahi kumtenda....basi anataka kufanya maamuzi magumu...lakini tena anakumbuka mahubiri na mafundisho ya ndoa aliyopitia....ndio ni mpaka kifo kitakapowatenganisha.

   Basi baada ya muda akawa amepata nguvu na ujasiri na akaadhimia na yeye kwenda kumshurutisha tena mumewe ili warudie tena na hiyo ilikuwa mida ya saa tisa usiku...Basi akatoka bafuni akiwa na taulo lake na hapo akamkuta muwewe amelalia mgongo na usingizi umeshamchukua...nae akajiambia nafsini mwake nitafungua pajama hii na kufanya kila juhudi na akiamka tu nakaa juu (Ikumbukwe kuwa  mpaka hapo Msichana huyu alikuwa hajaona sehemuza siri za mumewe, maana walipofika hotelini walioga tofauti tofauti, na hata mkaka alivyompandia mkewe,yule mdada alikuwa amelalia mgongo, hivyo hakuona kitu zaidi ya kuhisi tu)

    Basi yule mwanamke akavua taulo lake na kuweka kando, naam akabaki kama alivyozaliwa...na taratibu kabisa akamsogelea mumewe na kuanza kufungua ile kamba ya pajama taratibu, na alipoifungua akaanza kuivua/kuifunua hapo akiwa na macho ya hamu na woga, anagalau aone miliki yake laivu kwa macho yake, mara alivyofunua tu hivi na kumwacha mumewe Uchi kabisa....Binti alishtuka kwa mshangao na kusema "Mamaaaa" na hapo akaangukia kitandani na kuzimia......................ITAENDELEA!!!!


(Nini alichokiona mpaka ashtuke na kuzimia? Je nini kiliendelea baada ya hapo?...Usikose kufuatilia sehemu ya 4 ya ushuhuda huu wenye kukusaidia wewe msomaji kama utazingatia kwa makini)


@Kwa hisani kubwa ya http://quality-love.blogspot.com/ (c)2013
King Chavala-MC
+255 713 883 797

Sunday, July 28, 2013

LAWRANCE NA WEMA MWANTIMWA, IWE HAMSA KWA VIJANA WASIOA KUOA!!!!

 UPENDO WA KWELI UNATOKANA NA MUNGU, HII NI KWASABABU MUNGU MWENYEWE NI PENDO..HESHIMA YA KIPEKEE YA MAHUSIANO YOYOTE YALE NI KUHALALISHA NA KUWA RASMI MBELE YA MUNGU NA BINADAMU....SIO KAZI RAHISI KIBINADAMU NA WALA SIO YA KUKURUPUKA HATA KIDOGO, LAKINI KAMA UKIMWAMINI MUNGU LAZIMA UTATIMIZA YOTE UNAYOTAKA KUYATIMIZA.....VIJANA WENGI SANA KWA SASA WAKO KATIKA MICHAKATO YA KUOA NA KUOLEWA NA WENGINE WAMESHAMALIZA  NA SASA WANA MAISHA YAO

LEO KIPEKEE TUNAKULETEA PICHA CHACHE TU ZA KUMBUKUMBU YA HARUSI YA MR & MRS LAWRANCE AND WEMA MWANTIMWA ILIYOFUNGWA TAREHE 14TH APRIL 2013 PALE CITY HARVEST NA HATIMAYE TAFRIJA KUFANYIKA KATIKA BUSTANI YA MAKUMBUSHO YA JIJINI DAR ES SALAAM...HARUSI HIYO ILIYOKUWA YA KIPEKEE SANA CHINI YA MWENYEKITI NOEL TENGA NA KAMATI YAKE NA MAANDALIZI NA KUENDESHWA NA MA-MC SAMUEL SASALI PAMOJA NTOKE BABU, BASI HIZI NI PICHA CHACHE TU ZA HARUSI HIYO!!

NA WEWE ZIKUTIE HAMASA ILI UJIFUNZE NINI MAANA YA UPENDO WA KWELI NA HESHIMA YA KUOA ....KARIBU SANA!!!
 SIKU LAWRANCE ALIPOMVIKA WEMA PETE  YA UCHUMBA KATIKA KANISA LA CITY HARVEST,JIJINI DAR ES SALAAM!
MAHARUSI,WASIMAMIZI NA WAPAMBE WOTE
ULICHEZWA SANA UKUTI UKUTI WA KICHAGA

 NA HII PICHA YA PAMOJA YA WAPAMBE WA KIKE
SAFARI YA MAISHA NDIO IMEANZA NA FUTURE NDIO ILEEEEE....

Safi saaaana


Lawrance akimlisha mkewe.

Wema akimlisha Mumewe


MR & MRS LAWRANCE AND WEMA MWANTIMWA
KWA NIABA YA UONGOZI NA WAFANYAKAZI WOTE WA BLOG HII (QUALITY-LOVE BASE), NINAWATAKIENI MAISHA MEMA, MAZURI YENYE BARAKA TELE ZA NDOA, SAWASAWA NA MLIVYOPENDANA  NA KUAPIANA KANISANI MBELE YA MUNGU NA WANADAMU, BASI UPENDO KATI YENU UZIDI KUIMARIKA KILA SIKU,AMEN!

Hotline; +255 713 883 797

Wednesday, July 24, 2013

USIKU ULE WA KWANZA WA FUNGATE (HONEYMOON)-Part 2

kwa wale wenye kumbukumbu nzuri,nilianza kuwaletea habari moja toka huko kibaha na nilikuwa kimya kwa muda ili kupata habari kamili za yote yaliyojiri, naam kwa wale ambao hawakusoma iliyopita,ninawasahuri waanzie kwanza hapa kisha tuendelee

http://quality-love.blogspot.com/2013/06/usiku-ule-wa-kwanza-wa-fungatehoneymoon.html

.......Lakini baada ya miezi mitatu nilienda tena huko kibaha ili nijue nini kinaendelea katika sakata hilo na hapo ndio nikagundua kuwa kumbe yule kijana alikuwa..........ENDELEA Part 2

*********************************************************************************

...Mtumishi aliyetumika kanisani kwa kipindi kirefu pamoja na baba yake mzazi na binti huyu,na kijana huyu kwa jinsi alivyokuwa akijitoa na kwa namna alivyohudumu na mchungaji huyo kwa muda mrefu,alipendwa sana aitha kwa utani au kwa kumaanisha mchungaji amewahi kusema..."Nitakupa zawadi ya mke toka nyumbani kwangu" na kipindi hicho mama mzazi alisikia na aliamini hivyo, sema bahati mbaya sana Mchungaji alifariki kabla ya kushuhudia binti yake anaolewa na nani.

Kwa hakika kijana alilewa katika maadili ambayo hata mabadiliko ya sayansi na tekinolojia alikemea na kuona ni dhambi....kijana huyo hakupenda TV wala hakusoma magazeti,kwake Biblia na maombi vilitosha kabisa kujua ulimwengu unaendaje.
Bado haifahamiki kuwa kijana huyu amewahi au hajawahi kuwa na mahusiano au kufanya mapenzi hapo kabla ingawa amewahi kutengwa kwa.......(nitazungumzia hapo mbeleni).
Ila kwa taarifa za mama mzazi wa binti yule, nilizopata wakati akimfokea mwanae kwa kitendo alichokifanya ni kwamba, baada ya harusi tu wakiwa kwenye gari kwenda honeymoon Kijana huyo alianza kwa kumshikashika taratibu huku akishukuru binti huyo kuolewa na yeye,inavyoonyesha kijana huyo hakumshika kwa msukumo wa kimahaba ila kwa kupata hiyo nafasi ya kuwa nae karibu sana kwa mara ya kwanza, na kwahiyo binti joto likapanda sana na kwa kuwa alikuwa yuko na mume wake aliamini usiku ule utakuwa wa kihistoria na hii ni kwasababu ya siku ile kuwa mbaya kwake (High heat katika mzunguko wake), na kwa kuwa alikuwa hajafanya kwa muda mrefu (ikumbukwe kuwa binti huyu amewahi kukengeuka na kufanya ufuska sana kabla hajarejea kundini na hivyo uzoefu wa mtaani ulikuwa mkubwa sana) na zaidi ya yote alikuwa tayari ameanza kushikwashikwa, samahani kwa lugha ya wazi lakini nimetamani ujue ukweli wote yamkini na wewe ukakusaidia kwa namna moja ama nyingine.
Basi walipofika hapo hotelini,walishushiwa zawadi zao na wale wasimamizi wakateta nao kidogo kisha wakawaacha na kuondoka zao.

Basi walipobaki peke yao,yule binti alimrukia kijana kwa kumbato la kubembea na kisha akaanza romance,lakini kijana huyu hakuonekana kupendezwa na hilo labda kwasababu hakujua na hivyo alijitahidi kuvumilia lakini hatimaye akamshusha chini na kumwambia yaliyokuwa kichwani mwake, basi binti akakubali na kuanza kusikiliza huku joto likiwa juu vibaya mno,basi yule kijana akasema natamani tumshukuru Mungu kwanza kwa sisi kufanikiwa kufunga ndoa na tuweke mikononi mwa Mungu yoote yaliyo mbele yetu,basi wakapiga magoti kando ya kitanda (huku binti akiwa na hamu yale maombi yaishe haraka),basi kijana wa watu alianza kuomba na kushukuru,akazama na kuanza kunena sana....yule binti masikini akaona hii sio akaingia kuoga na kurudi amevaa taulu,lakini mtumishi alipomwona binti na taulo ndio akaanza kukemea mapepo masalia ya uzinzi ndani ya mke wake na kuomba sana,
Binti alipochoka kusubiri akajilaza kitandani kwa hasira na kwa sababu ya uchovu na hasira kajiusingizi kakampitia......na huku baada ya maombi ya mtumishi ya takribani masaa mawili, nae akaenda kuoga na kurudi akiwa na pajama na kumkuta mkewe amepitiwa na usingizi akiwa amelalia mgongo akiwa na Taulo tu, basi hivyohivyo Mtumishi huyo akaamua kum...........ITAENDELEA!!!

(Unaweza kuhisi mtumishi aliamua kufanya nini hivyohivyo?....usijali usikose mwendelezo wa hadithi ya kweli toka kibaha,ili ujifunze kwa faida yako!!)

@Kwa hisani kubwa ya http://quality-love.blogspot.com/ (c)2013
King Chavala-MC
+255 713 883 797

Thursday, July 18, 2013

#KATIKA KUTAFUTA MWENZA#....USITAFUTE ANAYEKUFAA, BALI JITAFUTE WEWE UNAPOFAA!!!!


Habari!
Ninaamini ninaongea na mtu mzima na timamu wa akili kabisa kichwani!
Ninakushukuru hata kwa kutenga muda wako wa kujifunza kwa kusoma hapa yamkini na huko kwingineko!!
Kila jambo chini ya jua lina KANUNI zake,na kanuni hizo zikifuatwa vema huwa tunatarajia matokeo mazuri lakini kama zikikiukwa basi madhara hayaepukiki!

Na kwa kuwa sisi tumezaliwa tukiwa hatujui kitu,imetupasa kujifunza kila kitu kwa kina illi tusivunje kanuni.

Sasa ambacho huwa kinanishangaza  ni kuwa yale mambo madogo madogo ambayo hayasumbui sana maishani huwa tunatumia juhudi kubwa sana kujifunza na kisha yanayogusa kabisa mioyo yetu tunafanya kimazoea na ndio maana wengi wanaumia,maana huwa tunajiamini na kufanya kana kwamba tunajua hali hatujui....na mbaya zaidi ni kuwa hatujui na hatujui kuwa hatujui....na kama haitoshi mtu anaweza kuwa na Doctrate degree lakini bado hapa akachemka na yule msukuma mkokoteni akaukata kwa kufurahia maisha yake safi ya mahusiano.

ZINGATIA SHULE HII;

1. ASIYEJUA ALIKOTOKA HAWEZI KUJUA ANAKOKWENDA
(Yaani asiyejijua yeye mwenyewe vema,hawezi kujua maishani mwake anahitaji nini hasa)

2.ASIYEJUA AENDAKO HUWA HAPOTEI NJIA
(Anayetafuta kwa nguvu ya macho huwa haridhiki na hataacha kutafuta)

Elimu yetu imetufundisha mambo mengi lakini imetuharibu mitazamo....yaani kila mmoja anajiona yeye yuko sahihi ila mwingine yeyote yule hayuko sana na tumeandaliwa kujifunza juu ya vitu vingine tu zaidi ya sisi wenyewe na tena kuvichunguza sana kwa bidii mno kabla ya kuvifanyia maamuzi.

Ndio maana mara zote watu huwa hawazingatii kujifahamu vema,kujijua tabia zao kwa kina,kuyajua madhaifu yako na hata kujifunza kurekebishika taratibu maana inawezekana....tunabaki kutafuta huyu na yule na kazi yetu inakuwa ni kukosoa tu tabia za wengine na kusahau kuwa kuna mengine wao hufanya kama kujikinga tu kwa zile tabia zao.

MFANO;
Inawezekana sana lakini ni ngumu mno kwa mtu mwenye TABIA KUU kuhusiana na mtu mwenye TABIA KUU  kama yeye i.e Mtu muongeaji sana hawezi kukaa kwa salama na muongeaji mwingine,mtu anayependa kutuma ama kuamrisha hawezi kukaa na mtu kama yeye,hivyo ni vema mtu wa TABIA KUU akawa na Mtu wa TABIA SAWIA.

Lakini jambo la msingi sana ambalo linapaswa kuzingatiwa ni hili;
USIHANGAIKE KUTAFUTA NANI ANAKUFAA,BALI JITAMBUE NA UJIFAHAMU VEMA NA HAPO UTAJUA KWA HAKIKA WAPI UNAFAA...Maana yamkini kila unayemtaka ni TOO GOOD FOR YOU!!! ama wewe YOU ARE TOO GOOD for HIM/HER!
Sasa nafikiri ubadilishe hata namna ya utafutaji wako na uombaji wako,vinginevyo utaangukia pua

UHALISIA; Unajua kuna watu wamerukaruka weeeee halafu sasa anamtaka mtu BIKIRA(Wa kiume au wa Kike)....why Mungu akupe wewe na asimpe anayemstahili?
Na wengine wako rafu rafu tu,lakini wanataka kuhusiana na watu walio smart sana,hapana haiwezekani umeshindwa kujitunza wewe mwenyewe na kisha leo Mungu akupe treasure yake ili nayo uichakaze....Ni kweli Mungu anatupenda sana na anatuwazia mema mno lakini hawezi akaruhuru Mtoto mchanga aendeshe Hammer maana itamuua tu japo mtoto anatamani aendeshe kama wakubwa!!

HIVYO MARAFIKI NINAWSIHI SANA USILAZIMISHE URAFIKI WALA MAHUSIANO KWASABABU TU UNAMTAKA YULE AMA HUYU,LAKINI ACHA KUWA NA MAAMUZI HURU NDANI YA NAFSI YA KILA MMOJA NA HAPO NDIO MTADUMU,VINGINEVYO UNAWEZA KWENDA DUKANI KUNUNUA NATI KWA KUBAHATISHA TU,LAKINI LAITI UKIJUA BOLTI YAKO NI SAIZI NGAPI NI RAHISI KUTAFUTA NATI HUSIKA PAMOJA SPANA YA KUKAZIA!!!

AHSANTENI

King Chavala-MC
+255 713 883 797

Wednesday, July 17, 2013

MR HENRY AND ANNETH KWIYEYA HAVE NOW STARTED THEIR JOURNEY!!!




Just like a dream but it is true that my friend Henry & Anneth have already started a new journey together...Wishing you all the best and all the blessing of God in your Marriage life!!!