Sunday, July 28, 2013

LAWRANCE NA WEMA MWANTIMWA, IWE HAMSA KWA VIJANA WASIOA KUOA!!!!

 UPENDO WA KWELI UNATOKANA NA MUNGU, HII NI KWASABABU MUNGU MWENYEWE NI PENDO..HESHIMA YA KIPEKEE YA MAHUSIANO YOYOTE YALE NI KUHALALISHA NA KUWA RASMI MBELE YA MUNGU NA BINADAMU....SIO KAZI RAHISI KIBINADAMU NA WALA SIO YA KUKURUPUKA HATA KIDOGO, LAKINI KAMA UKIMWAMINI MUNGU LAZIMA UTATIMIZA YOTE UNAYOTAKA KUYATIMIZA.....VIJANA WENGI SANA KWA SASA WAKO KATIKA MICHAKATO YA KUOA NA KUOLEWA NA WENGINE WAMESHAMALIZA  NA SASA WANA MAISHA YAO

LEO KIPEKEE TUNAKULETEA PICHA CHACHE TU ZA KUMBUKUMBU YA HARUSI YA MR & MRS LAWRANCE AND WEMA MWANTIMWA ILIYOFUNGWA TAREHE 14TH APRIL 2013 PALE CITY HARVEST NA HATIMAYE TAFRIJA KUFANYIKA KATIKA BUSTANI YA MAKUMBUSHO YA JIJINI DAR ES SALAAM...HARUSI HIYO ILIYOKUWA YA KIPEKEE SANA CHINI YA MWENYEKITI NOEL TENGA NA KAMATI YAKE NA MAANDALIZI NA KUENDESHWA NA MA-MC SAMUEL SASALI PAMOJA NTOKE BABU, BASI HIZI NI PICHA CHACHE TU ZA HARUSI HIYO!!

NA WEWE ZIKUTIE HAMASA ILI UJIFUNZE NINI MAANA YA UPENDO WA KWELI NA HESHIMA YA KUOA ....KARIBU SANA!!!
 SIKU LAWRANCE ALIPOMVIKA WEMA PETE  YA UCHUMBA KATIKA KANISA LA CITY HARVEST,JIJINI DAR ES SALAAM!
MAHARUSI,WASIMAMIZI NA WAPAMBE WOTE
ULICHEZWA SANA UKUTI UKUTI WA KICHAGA

 NA HII PICHA YA PAMOJA YA WAPAMBE WA KIKE
SAFARI YA MAISHA NDIO IMEANZA NA FUTURE NDIO ILEEEEE....

Safi saaaana


Lawrance akimlisha mkewe.

Wema akimlisha Mumewe


MR & MRS LAWRANCE AND WEMA MWANTIMWA
KWA NIABA YA UONGOZI NA WAFANYAKAZI WOTE WA BLOG HII (QUALITY-LOVE BASE), NINAWATAKIENI MAISHA MEMA, MAZURI YENYE BARAKA TELE ZA NDOA, SAWASAWA NA MLIVYOPENDANA  NA KUAPIANA KANISANI MBELE YA MUNGU NA WANADAMU, BASI UPENDO KATI YENU UZIDI KUIMARIKA KILA SIKU,AMEN!

Hotline; +255 713 883 797

Wednesday, July 24, 2013

USIKU ULE WA KWANZA WA FUNGATE (HONEYMOON)-Part 2

kwa wale wenye kumbukumbu nzuri,nilianza kuwaletea habari moja toka huko kibaha na nilikuwa kimya kwa muda ili kupata habari kamili za yote yaliyojiri, naam kwa wale ambao hawakusoma iliyopita,ninawasahuri waanzie kwanza hapa kisha tuendelee

http://quality-love.blogspot.com/2013/06/usiku-ule-wa-kwanza-wa-fungatehoneymoon.html

.......Lakini baada ya miezi mitatu nilienda tena huko kibaha ili nijue nini kinaendelea katika sakata hilo na hapo ndio nikagundua kuwa kumbe yule kijana alikuwa..........ENDELEA Part 2

*********************************************************************************

...Mtumishi aliyetumika kanisani kwa kipindi kirefu pamoja na baba yake mzazi na binti huyu,na kijana huyu kwa jinsi alivyokuwa akijitoa na kwa namna alivyohudumu na mchungaji huyo kwa muda mrefu,alipendwa sana aitha kwa utani au kwa kumaanisha mchungaji amewahi kusema..."Nitakupa zawadi ya mke toka nyumbani kwangu" na kipindi hicho mama mzazi alisikia na aliamini hivyo, sema bahati mbaya sana Mchungaji alifariki kabla ya kushuhudia binti yake anaolewa na nani.

Kwa hakika kijana alilewa katika maadili ambayo hata mabadiliko ya sayansi na tekinolojia alikemea na kuona ni dhambi....kijana huyo hakupenda TV wala hakusoma magazeti,kwake Biblia na maombi vilitosha kabisa kujua ulimwengu unaendaje.
Bado haifahamiki kuwa kijana huyu amewahi au hajawahi kuwa na mahusiano au kufanya mapenzi hapo kabla ingawa amewahi kutengwa kwa.......(nitazungumzia hapo mbeleni).
Ila kwa taarifa za mama mzazi wa binti yule, nilizopata wakati akimfokea mwanae kwa kitendo alichokifanya ni kwamba, baada ya harusi tu wakiwa kwenye gari kwenda honeymoon Kijana huyo alianza kwa kumshikashika taratibu huku akishukuru binti huyo kuolewa na yeye,inavyoonyesha kijana huyo hakumshika kwa msukumo wa kimahaba ila kwa kupata hiyo nafasi ya kuwa nae karibu sana kwa mara ya kwanza, na kwahiyo binti joto likapanda sana na kwa kuwa alikuwa yuko na mume wake aliamini usiku ule utakuwa wa kihistoria na hii ni kwasababu ya siku ile kuwa mbaya kwake (High heat katika mzunguko wake), na kwa kuwa alikuwa hajafanya kwa muda mrefu (ikumbukwe kuwa binti huyu amewahi kukengeuka na kufanya ufuska sana kabla hajarejea kundini na hivyo uzoefu wa mtaani ulikuwa mkubwa sana) na zaidi ya yote alikuwa tayari ameanza kushikwashikwa, samahani kwa lugha ya wazi lakini nimetamani ujue ukweli wote yamkini na wewe ukakusaidia kwa namna moja ama nyingine.
Basi walipofika hapo hotelini,walishushiwa zawadi zao na wale wasimamizi wakateta nao kidogo kisha wakawaacha na kuondoka zao.

Basi walipobaki peke yao,yule binti alimrukia kijana kwa kumbato la kubembea na kisha akaanza romance,lakini kijana huyu hakuonekana kupendezwa na hilo labda kwasababu hakujua na hivyo alijitahidi kuvumilia lakini hatimaye akamshusha chini na kumwambia yaliyokuwa kichwani mwake, basi binti akakubali na kuanza kusikiliza huku joto likiwa juu vibaya mno,basi yule kijana akasema natamani tumshukuru Mungu kwanza kwa sisi kufanikiwa kufunga ndoa na tuweke mikononi mwa Mungu yoote yaliyo mbele yetu,basi wakapiga magoti kando ya kitanda (huku binti akiwa na hamu yale maombi yaishe haraka),basi kijana wa watu alianza kuomba na kushukuru,akazama na kuanza kunena sana....yule binti masikini akaona hii sio akaingia kuoga na kurudi amevaa taulu,lakini mtumishi alipomwona binti na taulo ndio akaanza kukemea mapepo masalia ya uzinzi ndani ya mke wake na kuomba sana,
Binti alipochoka kusubiri akajilaza kitandani kwa hasira na kwa sababu ya uchovu na hasira kajiusingizi kakampitia......na huku baada ya maombi ya mtumishi ya takribani masaa mawili, nae akaenda kuoga na kurudi akiwa na pajama na kumkuta mkewe amepitiwa na usingizi akiwa amelalia mgongo akiwa na Taulo tu, basi hivyohivyo Mtumishi huyo akaamua kum...........ITAENDELEA!!!

(Unaweza kuhisi mtumishi aliamua kufanya nini hivyohivyo?....usijali usikose mwendelezo wa hadithi ya kweli toka kibaha,ili ujifunze kwa faida yako!!)

@Kwa hisani kubwa ya http://quality-love.blogspot.com/ (c)2013
King Chavala-MC
+255 713 883 797

Thursday, July 18, 2013

#KATIKA KUTAFUTA MWENZA#....USITAFUTE ANAYEKUFAA, BALI JITAFUTE WEWE UNAPOFAA!!!!


Habari!
Ninaamini ninaongea na mtu mzima na timamu wa akili kabisa kichwani!
Ninakushukuru hata kwa kutenga muda wako wa kujifunza kwa kusoma hapa yamkini na huko kwingineko!!
Kila jambo chini ya jua lina KANUNI zake,na kanuni hizo zikifuatwa vema huwa tunatarajia matokeo mazuri lakini kama zikikiukwa basi madhara hayaepukiki!

Na kwa kuwa sisi tumezaliwa tukiwa hatujui kitu,imetupasa kujifunza kila kitu kwa kina illi tusivunje kanuni.

Sasa ambacho huwa kinanishangaza  ni kuwa yale mambo madogo madogo ambayo hayasumbui sana maishani huwa tunatumia juhudi kubwa sana kujifunza na kisha yanayogusa kabisa mioyo yetu tunafanya kimazoea na ndio maana wengi wanaumia,maana huwa tunajiamini na kufanya kana kwamba tunajua hali hatujui....na mbaya zaidi ni kuwa hatujui na hatujui kuwa hatujui....na kama haitoshi mtu anaweza kuwa na Doctrate degree lakini bado hapa akachemka na yule msukuma mkokoteni akaukata kwa kufurahia maisha yake safi ya mahusiano.

ZINGATIA SHULE HII;

1. ASIYEJUA ALIKOTOKA HAWEZI KUJUA ANAKOKWENDA
(Yaani asiyejijua yeye mwenyewe vema,hawezi kujua maishani mwake anahitaji nini hasa)

2.ASIYEJUA AENDAKO HUWA HAPOTEI NJIA
(Anayetafuta kwa nguvu ya macho huwa haridhiki na hataacha kutafuta)

Elimu yetu imetufundisha mambo mengi lakini imetuharibu mitazamo....yaani kila mmoja anajiona yeye yuko sahihi ila mwingine yeyote yule hayuko sana na tumeandaliwa kujifunza juu ya vitu vingine tu zaidi ya sisi wenyewe na tena kuvichunguza sana kwa bidii mno kabla ya kuvifanyia maamuzi.

Ndio maana mara zote watu huwa hawazingatii kujifahamu vema,kujijua tabia zao kwa kina,kuyajua madhaifu yako na hata kujifunza kurekebishika taratibu maana inawezekana....tunabaki kutafuta huyu na yule na kazi yetu inakuwa ni kukosoa tu tabia za wengine na kusahau kuwa kuna mengine wao hufanya kama kujikinga tu kwa zile tabia zao.

MFANO;
Inawezekana sana lakini ni ngumu mno kwa mtu mwenye TABIA KUU kuhusiana na mtu mwenye TABIA KUU  kama yeye i.e Mtu muongeaji sana hawezi kukaa kwa salama na muongeaji mwingine,mtu anayependa kutuma ama kuamrisha hawezi kukaa na mtu kama yeye,hivyo ni vema mtu wa TABIA KUU akawa na Mtu wa TABIA SAWIA.

Lakini jambo la msingi sana ambalo linapaswa kuzingatiwa ni hili;
USIHANGAIKE KUTAFUTA NANI ANAKUFAA,BALI JITAMBUE NA UJIFAHAMU VEMA NA HAPO UTAJUA KWA HAKIKA WAPI UNAFAA...Maana yamkini kila unayemtaka ni TOO GOOD FOR YOU!!! ama wewe YOU ARE TOO GOOD for HIM/HER!
Sasa nafikiri ubadilishe hata namna ya utafutaji wako na uombaji wako,vinginevyo utaangukia pua

UHALISIA; Unajua kuna watu wamerukaruka weeeee halafu sasa anamtaka mtu BIKIRA(Wa kiume au wa Kike)....why Mungu akupe wewe na asimpe anayemstahili?
Na wengine wako rafu rafu tu,lakini wanataka kuhusiana na watu walio smart sana,hapana haiwezekani umeshindwa kujitunza wewe mwenyewe na kisha leo Mungu akupe treasure yake ili nayo uichakaze....Ni kweli Mungu anatupenda sana na anatuwazia mema mno lakini hawezi akaruhuru Mtoto mchanga aendeshe Hammer maana itamuua tu japo mtoto anatamani aendeshe kama wakubwa!!

HIVYO MARAFIKI NINAWSIHI SANA USILAZIMISHE URAFIKI WALA MAHUSIANO KWASABABU TU UNAMTAKA YULE AMA HUYU,LAKINI ACHA KUWA NA MAAMUZI HURU NDANI YA NAFSI YA KILA MMOJA NA HAPO NDIO MTADUMU,VINGINEVYO UNAWEZA KWENDA DUKANI KUNUNUA NATI KWA KUBAHATISHA TU,LAKINI LAITI UKIJUA BOLTI YAKO NI SAIZI NGAPI NI RAHISI KUTAFUTA NATI HUSIKA PAMOJA SPANA YA KUKAZIA!!!

AHSANTENI

King Chavala-MC
+255 713 883 797

Wednesday, July 17, 2013

MR HENRY AND ANNETH KWIYEYA HAVE NOW STARTED THEIR JOURNEY!!!




Just like a dream but it is true that my friend Henry & Anneth have already started a new journey together...Wishing you all the best and all the blessing of God in your Marriage life!!!




Thursday, June 27, 2013

VITU VYA MUHIMU VYA KUANGALIA UNAPOOMBA MWEZI WA MAISHA!!!!



hABARI ZENU!!!!
Watu wengi inapofika katika swala la kutafuta mwenzi wa maisha,nikiwa na maana mume au mke huwa inakuwa ngumu sana. Maana wanakuwa hawajui wafanye nini ili waweze kupata ubavu ambao ndio Mungu amekusudia na sio kuchukua ubavu wa wenzao. Ni jambo la maana sana unapotafuta au kujiandaa kuwa na mwenzi wa maisha kujua mambo muhimu yatakayo kusaidia kuepusha kukutana na mwenzi sahihi kutoka kwa Mungu.

Leo nitaelezea mambo muhimu matatu tu japo hii itakuwa series ambapo tutaendelea kueleza zaidi na zaidi juu ya vitu muhimu tunavyoendelea huko mbele.
Mambo hayo ni;
1.       Maombi
Maombi ni muhimu sana na yanakufanya uwe na ushirika na Mungu,na unapoomba ni ishara ya kumwambia Mungu kwamba bila wewe Mungu wangu siwezi. Kuna mchungaji mmoja alitufundisha ni muhimu kufanya maombi pale ambapo huna picha yoyote kichwani,maana tatizo la watu wengi ni kwamba wanakwenda kuomba Mungu huku ana picha ya mtu Fulani,au mwingine anamwambia Mungu ooh Mungu nipe huyu,nataka kukumbia rafiki hiyo sio njia nzuri.

Wewe muombe Mungu akupe mwenzi,halafu kama neno lake linavyosema kwamba tukiomba tuamini kwamba ametupatia na kwamba Mungu si dhalimu maana yeye ni baba atatupa kitu chema,basi tuamini hivyo.Ukishaomba na kuamini kwamba umepata hata kama katika hali halisi huoni anza kumshukuru Mungu kwa mwenzi mzuri kutoka kwake.

Mtumishi mwingine alifundisha unaweza kusema huyo mtu awe na haiba gani n.k,lakini ujue kwamba Mungu yuko juu ya vyote atakaye kupa ndio sahihi kuliko akili yako inavyohitaji au kudhani.

Maombi ni eneo muhimu sana ni vizuri ukawa na mtu ambaye mnaelewana na kiimani mko katika level moja au yeye amekuzidi mkawa mnaliombea hilo pamoja na mambo mengine yanayowazunguka,maana neno lake linasema palipo wawili watatu yeye yupo katikati yao,upako wa uwingi nao una umuhimu sana.

Unapukuwa katika maombi ni vizuri pia ukatubu maana unaweza ukawa na vitu vinavyozuia mawasiliano yako na Mungu. Tubu kwa chochote ambacho umefanya kwa kujua au kutojua maana Mungu wetu ni mtakatifu uende mbele zake ukiwa mweupe,Amen

2.       Je wewe ni mtu sahihi au unayefaa kuoa au kuolewa
Kitu kingine cha kuangalia nafikiri ni vizuri kujifanyia utafiti wewe mwenyewe,kujichunguza hivi kweli mimi kweli nina tabia gani ya kufaa kuishi na mtu mwingine.
 Hivi kweli mimi ninazo tabia za mke au mume mwema kweli ?
 Hivi mimi ni mtu ambaye watu wanaweza kumwamini na kumpa moyo wake kweli?

Ni kwanini nataka kuolewa au kuoa? Nataka kuolewa au kuoa  kwasababu mama au baba yangu anahitaji hivyo,au kwa vile rika langu wote wameolewa? Jamii inanionaje kwanza?
Ukijitafiti utagundua kwa njia moja au nyingine kuna mtu alishakupa mrudisho nyuma juu ya tabia zako mbaya,je kwa hizo tabia kweli bila kuzibadilisha kuna mtu anaweza kuishi na wewe? Jiulize peke yako wala usimuulize mtu,utapata majibu hayo utashangaa ambavyo unahitaji ujishughulikie kwanza. Watu wengi wanalia katika maombi oooh Mungu baba Jehova,naomba unipe mtu anayefaa kuwa mume au mke wangu lakini wao wanasahau hivi mimi Mungu ananionaje,kweli maisha yangu yanampa Mungu utukufu. Unaweza ukawa na vitabia ambavyo unaona kwamba si vibaya kumbe hivyo hivyo vyaweza kusimama kama kizingiti cha Baraka zako.
Ukishajua tatizo liko wapi badilika,saa nyingine kuna watu wanakuja na nia ya kuwa wenzi halafu wanaingia mitini basi ukijikagua unaona inawezekana tabia hii ndio imemkimbiza,basi vizuri kufanyia kazi na sio kukaa na kulia.
Kwakweli ni heri umlilie Mungu atakurehemu kuliko huyo aliyekukimbia maana akishaamua ndio ameamua na kama sio ubavu wako basi acha aende kwa ubavu wake,Amen

......TUTAENDELEA!!!! na somo hili,masomo haya yameandaliwa na Blogger wa Rejoice and Rejoice link http://rejoice-and-rejoice.blogspot.com/

Wednesday, June 19, 2013

"USIKU ULE WA KWANZA WA FUNGATE(HONEYMOON)"

UTANGULIZI;
Mwaka jana tulikwenda harusini huko kibaha,pwani na harusi kwa hakika ilipendeza kwa jinsi kamati ilivyojiandaa,naam shughuli ilikuwa motomoto kwasababu bibi harusi alikuwa ni binti pekee wa mchungaji,ambaye alikuwa anaishi tu na mama yake baada ya mchungaji kufariki dunia ajali ya majini akitoka kuhubiri injili huko visiwani mafia...na ilikuwa ni furaha pekee ya mama maana alisemwa mno kwasababu ya binti huyo,ndio binti huyo amewahi kukengeuka na kumtumikia shetani kwa kipindi fulani kabla hajarejea kundini.

KIINI CHA STORI;
Baada ya hizo shamla shamla na shamra shamra zote kukamilika basi sisi tulirejea makwetu tukiwatakia safari njema ya kwenda huko mwezini,na walipata bahati ya kwenda hoteli moja ya heshima tu inayotosha kabisa kufikia raha ya kilele cha huko mwezini bila bugudha!

N.B; Kwa kawaida makanisani kwetu huku watu hutakiwa kupima kwanza kabla ya kuona,lakini changamoto ni kuwa imekaririwa kuwa Ukimwi peke yake ndio inaweza kuwa kikwazo cha ndoa na tunasahau kuwa kuna magonjwa mengione kama vile sickle cells,magonjwa ya moyo,strelity hata size za maumbile ni muhimu kuwa na tahadhari in case kuna abnormalities)
...Sasa taarifa zilizotufikia ni kuwa baada ya kufika huko honeymoon,yule bibi harusi alifungasha saa kumi na moja asubuhi na kupotea huku akiacha kinote mezani....HAPANA,MIMI NAONA SIWEZI,NISAMEHE!
Na akamwandikia mama yake text hii..."Mama samahani,nitakuwa salama tu usinitafute,niliolewa ili furaha ya maisha iwe na heshima kwangu,ili niliokuta huku siwezi mama,bye" Na kisha akatuma line.
Yule Bwana harusi aliamua kurejea nyumbani akishindwa kusema hasa tatizo ni nini na nini kilitokea...na hivyo kuacha gumzo mtaani kote na kila alibaki kusema analohisi na kuona linafaa mdomoni kwake,wengine wakimsema mama mzazi kuwa alilazimisha ndoa,wengine wakisema binti hajatulia na hata wengine wakimsema huyu kijana wajuavyo.

   Lakini baada ya miezi mitatu nilienda tena huko kibaha ili nijue nini kinaendelea katika sakata hilo na hapo ndio nikagundua kuwa kumbe yule kijana alikuwa............ITAENDELEA!!!!!

(Unaweza ukajaribu kukisia niligundua nini huko,lakini hayo yatakuwa ni yako ukweli nitauleta mwenyewe)

@Kwa hisani kubwa ya http://quality-love.blogspot.com (c)2013
King Chavala-MC
+255 713 883 797

Monday, June 17, 2013

"29/09/2013".....OPEN LETTER TO ALL FROM KING CHAVALA!!!

MY FAITH & WISH(29/09/2013) Vs GOD'S BEST TIME OF GIVING ME A GIFT OF A WIFE....Mmmhhhhhhhhhh!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!?????????????????
*****************************************************
Hivi siku za karibuni nimekuwa nikipokea maswali na maulizo mengi sana,yaliyokaa katima mfumo wa uhojiji usio rasmi na kumbusho la habari ya hatma yangu ya "KUKAMILIKA"....na nimekaa kimya makusudi kwasababu kwa kadri nilivyoongea kila siku hata kama nimeongea haya ndani ya mwaka mmoja tu,watu wanaona kama niliaanza kuahidi miaka hiyoooo!
Anyway natamani niwajibuni nyote kwa pamoja kuwa VILE AMBAVYO NILISEMA,NDIO NILIMAANISHA KUMWAMINI BWANA KATIKA JAMBO HILI!.....unajua katika ulimwengu huu EVERYTHING IS DONE BY FAITH....Martin Luther King,amewahi kusema...You need not to see the whole staircase,just start the first step by faith!
***********************************************************

Pamoja na carrier yangu kama MC/Comedian,katika hili sijalifanyia utani,i was and i am very serious about it!.....But this issues need preparations na kuhusika kwa watu wengi sana,kwa mwezi wa pili mpaka wa nne tumepoteza 4 ndugu(Baba mkubwa,bibi mzaa baba,binamu na mjomba kaka wa mama) so kwa hali ya kawaida hakuna namna ningeanza process kwa hali hii,na zaidi ya hiyo in my church there are are some strictly steps and procedures to follow that are taged within 6months!
SO MY FAITH IS CONSTRAINED IN THIS NARROW PATH THOUGH I BELIEVE IN MIRACLES...The Bible says"Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu,bali jawabu la ulimi latoka kwa Bwana",so no way if at God is in Control mimi ni nani hata nibishane au nifanye tofauti ili tu kutunza promise yangu ya 29/09/2013 while God's time is the best time?
***********************************************************
Nilimwamini na bado namwamini Bwana kwa habari ya mwana-mwari asiye na kunyanzi lolote moyoni,naam nafsi yangu ikaona,lakini RIDHAA ya ayala yule haikuwa kwangu,yamkini nafsi zangu zilitafasiri vibaya ama labda sikufanya vema yaliyonipasa ama muda wake wa kupata kiuu bado mmmh! ni nani ajuaye siri za Bwana na akaenda kinyume na maagizo yake....yeye amezitukuza ahadi zake kuliko hata Jina lake,naam naamini itatimia kwangu!!
**********************************************************
NILITAMANI SANA NA BADO NATAMANI KUFANYA 29/09/2013 KAMA NILIKWISHA KUKIRI NA KUAMINI HIVYO,LAKINI IKIWA SITAPATA KIBALI CHA BWANA KWA SAA HIYO,SITAMLAUMU MUNGU HATA KIDOGO,KWA KUKWA KATIKA MAMBO YOTE YEYE HUFANYA KAZI NA WALE WAMPENDAO KATIKA KUWAPATIA MEMA!!
**********************************************************
Moyo wangu unaweza kuumia kumkosa binti yule hata sasa,lakini bado ninayo nafasi ya kuiambia nafsi yangu....PRAY FOR WHAT YOU DESERVE AND NOT WHAT YOU WANT(Maana yawezekana ukang'ang'ania kupata gari kumbe unastahili ndege,ama ukaomba treni sana kumbe unastahili kupata pikipiki....naam najua na ninaamini mke ni zawadi,Je ni nani mwenye utimamu kichwani ambaye huletewa zawadi na kabla hajaifungua akaambiwa zawadi yako sio hiyo bali ni hii na akapewa nyingine,nae akang'ang'ana kwa kusema...HAPANA MIMI NAITAKA HII,KWASABABU HII NDIO NZURI NA NIMESHAIZOEA MACHONI,hali hata hajui ndani kunani???)
Naam nimelazimika kuandika waraka huu kwenu,nyote wenye mapenzi mema na mimi na mnaniombea kheri ili msiache kuniombea kila siku maana huduma yangu ni kubwa na ni ya mataifa mengi,hivyo mke si jambo dogo wala la masikhara,hapa unamzungumzia mshauri na msaidizi wa "ICON OF AFRICA"
**********************************************************
MSINISUKUME WALA KUNISII KUOA ETI KWASABABU MARAFIKI ZANGU WENGI WAMEOA AU WANAOA,BALI MNISII NILITEGEE SHAURI LA BWANA NA KUONA KAMA YEYE AONAVYO!!!
**********************************************************
Kwa wale mliotendwa,kuachwa na kuumizwa,msione kama hapo ndio mwisho wa dunia,bali kaeni chini mjichunguze na kama kuna mahali kuna kosa basi jisahisheni na kusonga mbele,Biblia inasema.....Wakati wa Mazuri ufurahi,na wakati wa mabaya ufikiri,maana yote haya hutokea kwa kusudi!
Wakati mwingine hampati kwasababu mnang'angania mno vya zamani,au mnatafuta kwa lengo la kuwakomoa mliotendana nao,hiyo sio sawa!!
Msiache kuwapenda na kuwaombea wale waliowatenda ama hata wale wasiowapenda ninyi na huo ndio ukubwa.
********************************************************
Kwa wale mnaongoja kwa hamu harusi yangu,bado msichoke na wale wote walio kwenye michakato hivi sasa ya kuoa nawatakia kheri,hongereni kwa hatua na Mungu aimarishe mioyo yenu hasa katika kipindi hiki kisicho chepesi!
Namwamini Bwana kuwa saa ikifika basi mambo yote yatakuwa SAFIIII!
************************************************************
This are my words from my mind and my heart,if you are friend or fan or whatever,hit the "like" after reading and "share" if you wish!
I LOVE YOU AND I LOVE YOU SO MUCH!
Thank you!

Regards
King Chavala-MC
http://kingchavala.blogspot.com/